< Psalmorum 150 >

1 alleluia laudate Dominum in sanctis eius laudate eum in firmamento virtutis eius
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
2 laudate eum in virtutibus eius laudate eum secundum multitudinem magnitudinis eius
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 laudate eum in sono tubae laudate eum in psalterio et cithara
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
4 laudate eum in tympano et choro laudate eum in cordis et organo
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5 laudate eum in cymbalis bene sonantibus laudate eum in cymbalis iubilationis
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 omne quod spirat laudet Dominum alleluia
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!

< Psalmorum 150 >