< Psalmorum 116 >

1 alleluia dilexi quoniam exaudiet Dominus vocem orationis meae
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2 quia inclinavit aurem suam mihi et in diebus meis invocabo te
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
3 circumdederunt me dolores mortis pericula inferni invenerunt me tribulationem et dolorem inveni (Sheol h7585)
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
4 et nomen Domini invocavi o Domine libera animam meam
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
5 misericors Dominus et iustus et Deus noster miseretur
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6 custodiens parvulos Dominus humiliatus sum et liberavit me
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7 convertere anima mea in requiem tuam quia Dominus benefecit tibi
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8 quia eripuit animam meam de morte oculos meos a lacrimis pedes meos a lapsu
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9 placebo Domino in regione vivorum
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
10 alleluia credidi propter quod locutus sum ego autem humiliatus sum nimis
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
11 ego dixi in excessu meo omnis homo mendax
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
12 quid retribuam Domino pro omnibus quae retribuit mihi
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
13 calicem salutaris accipiam et nomen Domini invocabo
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
14 vota mea Domino reddam coram omni populo eius
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
15 pretiosa in conspectu Domini mors sanctorum eius
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
16 o Domine quia ego servus tuus ego servus tuus et filius ancillae tuae disrupisti vincula mea
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
17 tibi sacrificabo hostiam laudis et in nomine Domini invocabo
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
18 vota mea Domino reddam in conspectu omnis populi eius
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19 in atriis domus Domini in medio tui Hierusalem
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmorum 116 >