< Psalmorum 114 >

1 alleluia in exitu Israhel de Aegypto domus Iacob de populo barbaro
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 facta est Iudaea sanctificatio eius Israhel potestas eius
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 mare vidit et fugit Iordanis conversus est retrorsum
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 montes exultaverunt ut arietes colles sicut agni ovium
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 quid est tibi mare quod fugisti et tu Iordanis quia conversus es retrorsum
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 montes exultastis sicut arietes et colles sicut agni ovium
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 a facie Domini mota est terra a facie Dei Iacob
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 qui convertit petram in stagna aquarum et rupem in fontes aquarum
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psalmorum 114 >