< Job 32 >

1 omiserunt autem tres viri isti respondere Iob eo quod iustus sibi videretur
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 et iratus indignatusque Heliu filius Barachel Buzites de cognatione Ram iratus est autem adversus Iob eo quod iustum se esse diceret coram Deo
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 porro adversum amicos eius indignatus est eo quod non invenissent responsionem rationabilem sed tantummodo condemnassent Iob
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 igitur Heliu expectavit Iob loquentem eo quod seniores se essent qui loquebantur
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 cum autem vidisset quod tres respondere non potuissent iratus est vehementer
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 respondensque Heliu filius Barachel Buzites dixit iunior sum tempore vos autem antiquiores idcirco dimisso capite veritus sum indicare vobis meam sententiam
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 sperabam enim quod aetas prolixior loqueretur et annorum multitudo doceret sapientiam
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 sed ut video spiritus est in hominibus et inspiratio Omnipotentis dat intellegentiam
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 non sunt longevi sapientes nec senes intellegunt iudicium
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 ideo dicam audite me ostendam vobis etiam ego meam scientiam
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 expectavi enim sermones vestros audivi prudentiam vestram donec disceptaremini sermonibus
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 et donec putabam vos aliquid dicere considerabam sed ut video non est qui arguere possit Iob et respondere ex vobis sermonibus eius
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 ne forte dicatis invenimus sapientiam Deus proiecit eum non homo
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 nihil locutus est mihi et ego non secundum vestros sermones respondebo illi
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 extimuerunt non responderunt ultra abstuleruntque a se eloquia
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 quoniam igitur expectavi et non sunt locuti steterunt nec responderunt ultra
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 respondebo et ego partem meam et ostendam scientiam meam
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 plenus sum enim sermonibus et coartat me spiritus uteri mei
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 en venter meus quasi mustum absque spiraculo quod lagunculas novas disrumpit
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 loquar et respirabo paululum aperiam labia mea et respondebo
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 non accipiam personam viri et Deum homini non aequabo
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 nescio enim quamdiu subsistam et si post modicum tollat me factor meus
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.

< Job 32 >