< Job 13 >

1 ecce omnia et vidit oculus meus et audivit auris mea et intellexi singula
Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
2 secundum scientiam vestram et ego novi nec inferior vestri sum
Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
3 sed tamen ad Omnipotentem loquar et disputare cum Deo cupio
Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
4 prius vos ostendens fabricatores mendacii et cultores perversorum dogmatum
Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
5 atque utinam taceretis ut putaremini esse sapientes
Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
6 audite ergo correptiones meas et iudicium labiorum meorum adtendite
Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
7 numquid Deus indiget vestro mendacio ut pro illo loquamini dolos
Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
8 numquid faciem eius accipitis et pro Deo iudicare nitimini
Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
9 aut placebit ei quem celare nihil potest aut decipietur ut homo vestris fraudulentiis
Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
10 ipse vos arguet quoniam in abscondito faciem eius accipitis
Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
11 statim ut se commoverit turbabit vos et terror eius inruet super vos
Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
12 memoria vestra conparabitur cineri et redigentur in lutum cervices vestrae
Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
13 tacete paulisper ut loquar quodcumque mihi mens suggesserit
Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
14 quare lacero carnes meas dentibus meis et animam meam porto in manibus meis
Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
15 etiam si occiderit me in ipso sperabo verumtamen vias meas in conspectu eius arguam
Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
16 et ipse erit salvator meus non enim veniet in conspectu eius omnis hypocrita
Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
17 audite sermonem meum et enigmata percipite auribus vestris
Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
18 si fuero iudicatus scio quod iustus inveniar
Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
19 quis est qui iudicetur mecum veniat quare tacens consumor
Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
20 duo tantum ne facias mihi et tunc a facie tua non abscondar
Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
21 manum tuam longe fac a me et formido tua non me terreat
Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
22 et voca me et respondebo tibi aut certe loquar et tu responde mihi
Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
23 quantas habeo iniquitates et peccata scelera mea et delicta ostende mihi
Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24 cur faciem tuam abscondis et arbitraris me inimicum tuum
Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
25 contra folium quod vento rapitur ostendis potentiam tuam et stipulam siccam persequeris
Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
26 scribis enim contra me amaritudines et consumere me vis peccatis adulescentiae meae
Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
27 posuisti in nervo pedem meum et observasti omnes semitas meas et vestigia pedum meorum considerasti
Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
28 qui quasi putredo consumendus sum et quasi vestimentum quod comeditur a tinea
japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.

< Job 13 >