< Thessalonicenses I 5 >

1 De temporibus autem, et momentis fratres non indigetis ut scribamus vobis.
Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
2 Ipsi enim diligenter scitis quia dies Domini, sicut fur in nocte, ita veniet.
Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
3 cum enim dixerint pax, et securitas: tunc repentinus eis superveniet interitus, sicut dolor in utero habentis, et non effugient.
Watu watakapokuwa wanasema: “Kila kitu ni shwari na salama” ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
4 Vos autem fratres non estis in tenebris, ut vos dies illa tamquam fur comprehendat:
Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
5 omnes enim vos filii lucis estis, et filii diei: non sumus noctis, neque tenebrarum.
Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
6 Igitur non dormiamus sicut et ceteri, sed vigilemus, et sobrii simus.
Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
7 Qui enim dormiunt, nocte dormiunt: et qui ebrii sunt, nocte ebrii sunt.
Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
8 Nos autem, qui diei sumus, sobrii simus, induti loricam fidei, et charitatis, et galeam spem salutis:
Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
9 quoniam non posuit nos Deus in iram, sed in acquisitionem salutis per Dominum nostrum Iesum Christum,
Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
10 qui mortuus est pro nobis: ut sive vigilemus, sive dormiamus, simul cum illo vivamus.
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
11 Propter quod consolamini invicem: et aedificate alterutrum, sicut et facitis.
Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
12 Rogamus autem vos fratres ut noveritis eos, qui laborant inter vos, et praesunt vobis in Domino, et monent vos,
Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
13 ut habeatis illos abundantius in charitate propter opus illorum: et pacem habete cum eis.
Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
14 Rogamus autem vos fratres, corripite inquietos, consolamini pusillanimes, suscipite infirmos, patientes estote ad omnes.
Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
15 Videte ne quis malum pro malo alicui reddat: sed semper quod bonum est sectamini in invicem, et in omnes.
Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
16 Semper gaudete.
Furahini daima,
17 Sine intermissione orate.
salini kila wakati
18 In omnibus gratias agite: haec est enim voluntas Dei in Christo Iesu in omnibus vobis.
na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
19 Spiritum nolite extinguere.
Msimpinge Roho Mtakatifu;
20 Prophetias nolite spernere.
msidharau unabii.
21 Omnia autem probate: quod bonum est tenete.
Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
22 Ab omni specie mala abstinete vos:
na epukeni kila aina ya uovu.
23 Ipse autem Deus pacis sanctificet vos per omnia: ut integer spiritus vester, et anima, et corpus sine querela in adventu Domini nostri Iesu Christi conservetur.
Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu—roho, mioyo na miili yenu—mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Fidelis est, qui vocavit vos: qui etiam faciet.
Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
25 Fratres orate pro nobis.
Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
26 Salutate fratres omnes in osculo sancto.
Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
27 Adiuro vos per Dominum ut legatur epistola haec omnibus sanctis fratribus.
Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
28 Gratia Domini nostri Iesu Christi vobiscum. Amen.
Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< Thessalonicenses I 5 >