< Psalmorum 3 >

1 Psalmus David, Cum fugeret a facie Absalom filii sui. Domine quid multiplicati sunt qui tribulant me? multi insurgunt adversum me.
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 Multi dicunt animæ meæ: Non est salus ipsi in Deo eius.
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 Tu autem Domine susceptor meus es, gloria mea, et exaltans caput meum.
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 Voce mea ad Dominum clamavi: et exaudivit me de monte sancto suo.
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 Ego dormivi, et soporatus sum: et exurrexi, quia Dominus suscepit me.
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 Non timebo millia populi circumdantis me: exurge Domine: salvum me fac Deus meus.
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 Quoniam tu percussisti omnes adversantes mihi sine causa: dentes peccatorum contrivisti.
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Domini est salus: et super populum tuum benedictio tua.
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.

< Psalmorum 3 >