< Psalmorum 22 >

1 In finem pro susceptione matutina, Psalmus David. Deus Deus meus respice in me: quare me dereliquisti? longe a salute mea verba delictorum meorum.
Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali na wokovu wangu na mbali na maneno yangu yenye uchungu?
2 Deus meus clamabo per diem, et non exaudies: et nocte, et non ad insipientiam mihi.
Mungu wangu, ninalia mchana kutwa, lakini haunijibu, na wakati wa usiku sinyamazi!
3 Tu autem in sancto habitas, Laus Israel.
Bado wewe ni mtakatifu; wewe umekaa kama mfalme pamoja na sifa za Israeli.
4 In te speraverunt patres nostri: speraverunt, et liberasti eos.
Mababu zetu walikuamini wewe, na wewe uliwaokoa wao.
5 Ad te clamaverunt, et salvi facti sunt: in te speraverunt, et non sunt confusi.
Walikulilia wewe nao waka okolewa. Wao walikuamini wewe na hawakuvunjwa moyo.
6 Ego autem sum vermis, et non homo: opprobrium hominum, et abiectio plebis.
Bali mimi ni funza na sio mtu, nisiye faa kwa ubinadamu na hudharauliwa na watu.
7 Omnes videntes me, deriserunt me: locuti sunt labiis, et moverunt caput.
Wale wote wanionao hunisuta; hunidhihaki; hunitikisia vichwa vyao.
8 Speravit in Domino, eripiat eum: salvum faciat eum, quoniam vult eum.
Wao husema, “Yeye anamwamini Yahwe; mwache Yahwe amuokoe. Mwache amuokoe yeye, kwa kuwa yeye anampendeza sana Yeye.”
9 Quoniam tu es, qui extraxisti me de ventre: spes mea ab uberibus matris meæ.
Kwa kuwa wewe ulinileta kutoka tumboni; wewe ulinifanya nikuamini wewe wakati nikiwa nanyonya matiti ya mama yangu.
10 In te proiectus sum ex utero: de ventre matris meæ Deus meus es tu,
Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11 ne discesseris a me: Quoniam tribulatio proxima est: quoniam non est qui adiuvet.
Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12 Circumdederunt me vituli multi: tauri pingues obsederunt me.
Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13 Aperuerunt super me os suum, sicut leo rapiens et rugiens.
Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14 Sicut aqua effusus sum: et dispersa sunt omnia ossa mea. Factum est cor meum tamquam cera liquescens in medio ventris mei.
Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15 Aruit tamquam testa virtus mea, et lingua mea adhæsit faucibus meis: et in pulverem mortis deduxisti me.
Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16 Quoniam circumdederunt me canes multi: concilium malignantium obsedit me. Foderunt manus meas et pedes meos:
Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17 dinumeraverunt omnia ossa mea. Ipsi vero consideraverunt et inspexerunt me:
Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18 diviserunt sibi vestimenta mea, et super vestem meam miserunt sortem.
Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19 Tu autem Domine ne elongaveris auxilium tuum a me: ad defensionem meam conspice.
Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20 Erue a framea Deus animam meam: et de manu canis unicam meam:
Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21 Salva me ex ore leonis: et a cornibus unicornium humilitatem meam.
Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22 Narrabo nomen tuum fratribus meis: in medio ecclesiæ laudabo te.
Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.
23 Qui timetis Dominum laudate eum: universum semen Iacob glorificate eum:
Ninyi mnao mwogopa Yahwe, msifuni yeye! Ninyi nyote kizazi cha Yakobo, muheshimuni yeye! Simameni katika hofu yake, ninyi nyote kizazi cha Israeli!
24 Timeat eum omne semen Israel: quoniam non sprevit, neque despexit deprecationem pauperis: Nec avertit faciem suam a me: et cum clamarem ad eum exaudivit me.
Kwa kuwa haja dharau au kuchukia mateso ya aliye taabishwa; Yahwe hajamficha uso wake yeye; pindi wale walio taabishwa walipo mlilia yeye, yeye alisikia.
25 Apud te laus mea in ecclesia magna: vota mea reddam in conspectu timentium eum.
Yahwe, katika kusanyiko la watu wako nitakusifu kwa yale uliyo tenda; nami nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wanao muhofu yeye.
26 Edent pauperes, et saturabuntur: et laudabunt Dominum qui requirunt eum: vivent corda eorum in sæculum sæculi.
Walio onewa watakula na kutosheka; wale ambao humtafuta Yahwe watamsifu yeye. Mioyo yenu iishi milele.
27 Reminiscentur et convertentur ad Dominum universi fines terræ: Et adorabunt in conspectu eius universæ familiæ Gentium.
Watu wote wa duniani watakumbuka na kumrudia Yahwe; familia zote za mataifa watapiga magoti chini mbele yako.
28 Quoniam Domini est regnum: et ipse dominabitur Gentium.
Kwa kuwa utawala ni wa Yahwe; yeye ni mtawala wa mataifa.
29 Manducaverunt et adoraverunt omnes pingues terræ: in conspectu eius cadent omnes qui descendunt in terram.
Watu wote wa duniani waliofanikiwa wata sherekea na wata abudu; wale wote washukao katika mavumbi watapiga magoti mbele zake, wale ambao hawawezi kulinda maisha yao wenyewe.
30 Et anima mea illi vivet: et semen meum serviet ipsi.
Kizazi kijacho kitamtumikia yeye; wao watakiambia kizazi kinachofuatia kuhusu Bwana.
31 Annunciabitur Domino generatio ventura: et annunciabunt cæli iustitiam eius populo qui nascetur, quem fecit Dominus.
Wao watakuja na kuzungumza kuhusu haki yake; wao watawaambia watu ambao bado hawaja zaliwa yale ambayo Yahwe ameyafanya!

< Psalmorum 22 >