< Psalmorum 128 >

1 Canticum graduum. Beati omnes, qui timent Dominum, qui ambulant in viis eius.
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
2 Labores manuum tuarum quia manducabis: beatus es, et bene tibi erit.
Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Uxor tua sicut vitis abundans, in lateribus domus tuæ. Filii tui sicut novellæ olivarum, in circuitu mensæ tuæ.
Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
4 Ecce sic benedicetur homo, qui timet Dominum.
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
5 Benedicat tibi Dominus ex Sion: et videas bona Ierusalem omnibus diebus vitæ tuæ.
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 Et videas filios filiorum tuorum, pacem super Israel.
nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.

< Psalmorum 128 >