< Psalmorum 85 >

1 In finem, filiis Core, Psalmus. Benedixisti Domine terram tuam: avertisti captivitatem Iacob.
Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2 Remisisti iniquitatem plebis tuæ: operuisti omnia peccata eorum.
Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
3 Mitigasti omnem iram tuam: avertisti ab ira indignationis tuæ.
Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4 Converte nos Deus salutaris noster: et averte iram tuam a nobis.
Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5 Numquid in æternum irasceris nobis? aut extendes iram tuam a generatione in generationem?
Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6 Deus tu conversus vivificabis nos: et plebs tua lætabitur in te.
Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
7 Ostende nobis Domine misericordiam tuam: et salutare tuum da nobis.
Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
8 Audiam quid loquatur in me Dominus Deus: quoniam loquetur pacem in plebem suam. Et super sanctos suos: et in eos, qui convertuntur ad cor.
Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
9 Verumtamen prope timentes eum salutare ipsius: ut inhabitet gloria in terra nostra.
Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
10 Misericordia, et veritas obviaverunt sibi: iustitia, et pax osculatæ sunt.
Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
11 Veritas de terra orta est: et iustitia de cælo prospexit.
Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
12 Etenim Dominus dabit benignitatem: et terra nostra dabit fructum suum.
Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
13 Iustitia ante eum ambulabit: et ponet in via gressus suos.
Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.

< Psalmorum 85 >