< Psalmorum 69 >

1 In finem, pro iis, qui commutabuntur, David. Salvum me fac Deus: quoniam intraverunt aquæ usque ad animam meam.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 Infixus sum in limo profundi: et non est substantia. Veni in altitudinem maris: et tempestas demersit me.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 Laboravi clamans, raucæ factæ sunt fauces meæ: defecerunt oculi mei, dum spero in Deum meum.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Multiplicati sunt super capillos capitis mei, qui oderunt me gratis. Confortati sunt qui persecuti sunt me inimici mei iniuste: quæ non rapui, tunc exolvebam.
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Deus tu scis insipientiam meam: et delicta mea a te non sunt abscondita.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Non erubescant in me qui expectant te Domine, Domine virtutum. Non confundantur super me qui quærunt te, Deus Israel.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Quoniam propter te sustinui opprobrium: operuit confusio faciem meam.
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 Extraneus factus sum fratribus meis, et peregrinus filiis matris meæ.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Quoniam zelus domus tuæ comedit me: et opprobria exprobrantium tibi, ceciderunt super me.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 Et operui in ieiunio animam meam: et factum est in opprobrium mihi.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 Et posui vestimentum meum cilicium: et factus sum illis in parabolam.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Adversum me loquebantur qui sedebant in porta: et in me psallebant qui bibebant vinum.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Ego vero orationem meam ad te Domine: tempus beneplaciti Deus. In multitudine misericordiæ tuæ exaudi me, in veritate salutis tuæ:
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Eripe me de luto, ut non infigar: libera me ab iis, qui oderunt me, et de profundis aquarum.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Non me demergat tempestas aquæ, neque absorbeat me profundum: neque urgeat super me puteus os suum.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Exaudi me Domine, quoniam benigna est misericordia tua: secundum multitudinem miserationum tuarum respice in me.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Et ne avertas faciem tuam a puero tuo: quoniam tribulor, velociter exaudi me.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Intende animæ meæ, et libera eam: propter inimicos meos eripe me.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Tu scis improperium meum, et confusionem meam, et reverentiam meam.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 In conspectu tuo sunt omnes qui tribulant me, improperium expectavit cor meum et miseriam. Et sustinui qui simul contristaretur, et non fuit: et qui consolaretur, et non inveni.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Et dederunt in escam meam fel: et in siti mea potaverunt me aceto.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Fiat mensa eorum coram ipsis in laqueum, et in retributiones, et in scandalum.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Obscurentur oculi eorum ne videant: et dorsum eorum semper incurva.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Effunde super eos iram tuam: et furor iræ tuæ comprehendat eos.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 Fiat habitatio eorum deserta: et in tabernaculis eorum non sit qui inhabitet.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Quoniam quem tu percussisti, persecuti sunt: et super dolorem vulnerum meorum addiderunt.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Appone iniquitatem super iniquitatem eorum: et non intrent in iustitiam tuam.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Deleantur de Libro viventium: et cum iustis non scribantur.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Ego sum pauper et dolens: salus tua Deus suscepit me.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Laudabo nomen Dei cum cantico: et magnificabo eum in laude:
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 Et placebit Deo super vitulum novellum: cornua producentem et ungulas.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Videant pauperes et lætentur: quærite Deum, et vivet anima vestra:
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Quoniam exaudivit pauperes Dominus: et vinctos suos non despexit.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Laudent illum cæli et terra, mare, et omnia reptilia in eis.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 Quoniam Deus salvam faciet Sion: et ædificabuntur civitates Iuda. Et inhabitabunt ibi, et hereditate acquirent eam.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 Et semen servorum eius possidebit eam, et qui diligunt nomen eius, habitabunt in ea.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Psalmorum 69 >