< Psalmorum 49 >

1 In finem, filiis Core Psalmus. Audite hæc omnes gentes: auribus percipite omnes, qui habitatis orbem:
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Quique terrigenæ, et filii hominum: simul in unum dives et pauper.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 Os meum loquetur sapientiam: et meditatio cordis mei prudentiam.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 Inclinabo in parabolam aurem meam: aperiam in psalterio propositionem meam.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Cur timebo in die mala? iniquitas calcanei mei circumdabit me:
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 Qui confidunt in virtute sua: et in multitudine divitiarum suarum gloriantur.
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 Frater non redimit, redimet homo: non dabit Deo placationem suam.
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 Et pretium redemptionis animæ suæ: et laborabit in æternum,
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 et vivet adhuc in finem.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 Non videbit interitum, cum viderit sapientes morientes: simul insipiens, et stultus peribunt. Et relinquent alienis divitias suas:
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 et sepulchra eorum domus illorum in æternum. Tabernacula eorum in progenie, et progenie: vocaverunt nomina sua in terris suis.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 Et homo, cum in honore esset, non intellexit: comparatus est iumentis insipientibus, et similis factus est illis.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 Hæc via illorum scandalum ipsis: et postea in ore suo complacebunt.
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Sicut oves in inferno positi sunt: mors depascet eos. Et dominabuntur eorum iusti in matutino: et auxilium eorum veterascet in inferno a gloria eorum. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 Verumtamen Deus redimet animam meam de manu inferi, cum acceperit me. (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 Ne timueris cum dives factus fuerit homo: et cum multiplicata fuerit gloria domus eius.
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 Quoniam cum interierit, non sumet omnia: neque descendet cum eo gloria eius.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 Quia anima eius in vita ipsius benedicetur: confitebitur tibi cum benefeceris ei.
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 Introibit usque in progenies patrum suorum: et usque in æternum non videbit lumen.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 Homo, cum in honore esset, non intellexit: comparatus est iumentis insipientibus, et similis factus est illis.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Psalmorum 49 >