< Proverbiorum 8 >

1 Numquid non sapientia clamitat, et prudentia dat vocem suam?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 In summis, excelsisque verticibus supra viam, in mediis semitis stans,
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 iuxta portas civitatis in ipsis foribus loquitur, dicens:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 O viri, ad vos clamito, et vox mea ad filios hominum.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Intelligite parvuli astutiam, et insipientes animadvertite.
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Audite, quoniam de rebus magnis locutura sum: et aperientur labia mea, ut recta prædicent.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Veritatem meditabitur guttur meum, et labia mea detestabuntur impium.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Iusti sunt omnes sermones mei, non est in eis pravum quid, neque perversum.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Recti sunt intelligentibus, et æqui invenientibus scientiam.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Accipite disciplinam meam, et non pecuniam: doctrinam magis, quam aurum eligite.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Melior est enim sapientia cunctis pretiosissimis: et omne desiderabile ei non potest comparari.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Ego sapientia habito in consilio, et eruditis intersum cogitationibus.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Timor Domini odit malum: arrogantiam, et superbiam, et viam pravam, et os bilingue detestor.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Meum est consilium, et æquitas, mea est prudentia, mea est fortitudo.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Per me reges regnant, et legum conditores iusta decernunt:
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Per me principes imperant, et potentes decernunt iustitiam.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Ego diligentes me diligo: et qui mane vigilant ad me, invenient me.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Mecum sunt divitiæ, et gloria, opes superbæ, et iustitia.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Melior est enim fructus meus auro, et lapide pretioso, et genimina me argento electo.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 In viis iustitiæ ambulo, in medio semitarum iudicii,
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 ut ditem diligentes me, et thesauros eorum repleam.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 Dominus possedit me in initio viarum suarum, antequam quidquam faceret a principio.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Ab æterno ordinata sum, et ex antiquis antequam terra fieret.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Nondum erant abyssi, et ego iam concepta eram: necdum fontes aquarum eruperant:
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 necdum montes gravi mole constiterant: ante colles ego parturiebar:
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 adhuc terram non fecerat, et flumina, et cardines orbis terræ.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Quando præparabat cælos, aderam: quando certa lege, et gyro vallabat abyssos:
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 quando æthera firmabat sursum, et librabat fontes aquarum:
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 quando circumdabat mari terminum suum, et legem ponebat aquis, ne transirent fines suos: quando appendebat fundamenta terræ:
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 Cum eo eram cuncta componens: et delectabar per singulos dies, ludens coram eo omni tempore;
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 ludens in orbe terrarum: et deliciæ meæ esse, cum filiis hominum.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Nunc ergo filii audite me: Beati, qui custodiunt vias meas.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Audite disciplinam, et estote sapientes, et nolite abiicere eam.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Beatus homo qui audit me, et qui vigilat ad fores meas quotidie, et observat ad postes ostii mei.
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Qui me invenerit, inveniet vitam, et hauriet salutem a Domino:
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 qui autem in me peccaverit, lædet animam suam. Omnes, qui me oderunt, diligunt mortem.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.

< Proverbiorum 8 >