< Proverbiorum 25 >

1 Hæ quoque parabolæ Salomonis, quas transtulerunt viri Ezechiæ regis Iuda.
Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2 Gloria Dei est celare verbum, et gloria regum investigare sermonem.
Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
3 Cælum sursum, et terra deorsum, et cor regum inscrutabile.
Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
4 Aufer rubiginem de argento, et egredietur vas purissimum:
Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
5 Aufer impietatem de vultu regis, et firmabitur iustitia thronus eius.
Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
6 Ne gloriosus appareas coram rege, et in loco magnorum ne steteris.
Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
7 Melius est enim ut dicatur tibi: Ascende huc; quam ut humilieris coram principe.
Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
8 Quæ viderunt oculi tui, ne proferas in iurgio cito: ne postea emendare non possis, cum dehonestaveris amicum tuum.
Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
9 Causam tuam tracta cum amico tuo, et secretum extraneo ne reveles:
Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
10 ne forte insultet tibi cum audierit, et exprobrare non cesset. Gratia et amicitia liberant: quas tibi serva, ne exprobrabilis fias.
au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
11 Mala aurea in lectis argenteis, qui loquitur verbum in tempore suo.
Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
12 Inauris aurea, et margaritum fulgens, qui arguit sapientem, et aurem obedientem.
Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
13 Sicut frigus nivis in die messis, ita legatus fidelis ei, qui misit eum, animam ipsius requiescere facit.
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
14 Nubes, et ventus, et pluviæ non sequentes, vir gloriosus, et promissa non complens.
Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
15 Patientia lenietur princeps, et lingua mollis confringet duritiam.
Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
16 Mel invenisti, comede quod sufficit tibi, ne forte satiatus evomas illud.
Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
17 Subtrahe pedem tuum de domo proximi tui, nequando satiatus oderit te.
Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
18 Iaculum, et gladius, et sagitta acuta, homo qui loquitur contra proximum suum falsum testimonium.
Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
19 Dens putridus, et pes lassus, qui sperat super infideli in die angustiæ,
Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20 et amittit pallium in die frigoris. Acetum in nitro, qui cantat carmina cordi pessimo. Sicut tinea vestimento, et vermis ligno: ita tristitia viri nocet cordi.
Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21 Si esurierit inimicus tuus, ciba illum: si sitierit, da ei aquam bibere:
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22 prunas enim congregabis super caput eius, et Dominus reddet tibi.
maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23 Ventus aquilo dissipat pluvias, et facies tristis linguam detrahentem.
Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24 Melius est sedere in angulo domatis, quam cum muliere litigiosa, et in domo communi.
Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25 Aqua frigida animæ sitienti, et nuncius bonus de terra longinqua.
Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Fons turbatus pede, et vena corrupta, iustus cadens coram impio.
Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27 Sicut qui mel multum comedit, non est ei bonum: sic qui scrutator est maiestatis, opprimetur a gloria.
Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28 Sicut urbs patens et absque murorum ambitu, ita vir, qui non potest in loquendo cohibere spiritum suum.
Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.

< Proverbiorum 25 >