< Proverbiorum 16 >

1 Hominis est animam præparare: et Domini gubernare linguam.
Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
2 Omnes viæ hominis patent oculis eius: spirituum ponderator est Dominus.
Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
3 Revela Domino opera tua, et dirigentur cogitationes tuæ.
Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 Universa propter semetipsum operatus est Dominus: impium quoque ad diem malum.
Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 Abominatio Domini est omnis arrogans: etiam si manus ad manum fuerit, non est innocens. Initium viæ bonæ, facere iustitiam: accepta est autem apud Deum magis, quam immolare hostias.
Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 Misericordia et veritate redimitur iniquitas: et in timore Domini declinatur a malo.
Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 Cum placuerint Domino viæ hominis, inimicos quoque eius convertet ad pacem.
Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 Melius est parum cum iustitia, quam multi fructus cum iniquitate.
Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 Cor hominis disponit viam suam: sed Domini est dirigere gressus eius.
Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10 Divinatio in labiis regis, in iudicio non errabit os eius.
Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11 Pondus et statera iudicia Domini sunt: et opera eius omnes lapides sacculi.
Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
12 Abominabiles regi qui agunt impie: quoniam iustitia firmatur solium.
Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
13 Voluntas regum labia iusta: qui recta loquitur, diligetur:
Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
14 Indignatio regis, nuncii mortis: et vir sapiens placabit eam.
Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
15 In hilaritate vultus regis, vita: et clementia eius quasi imber serotinus.
Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
16 Posside sapientiam, quia auro melior est: et acquire prudentiam, quia pretiosior est argento.
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
17 Semita iustorum declinat mala: custos animæ suæ servat viam suam.
Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
18 Contritionem præcedit superbia: et ante ruinam exaltatur spiritus.
Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 Melius est humiliari cum mitibus, quam dividere spolia cum superbis.
Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 Eruditus in verbo reperiet bona: et qui sperat in Domino, beatus est.
Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 Qui sapiens est corde, appellabitur prudens: et qui dulcis eloquio, maiora percipiet.
Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 Fons vitæ eruditio possidentis: doctrina stultorum fatuitas.
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 Cor sapientis erudiet os eius: et labiis eius addet gratiam.
Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 Favus mellis, composita verba: dulcedo animæ, sanitas ossium.
Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 Est via quæ videtur homini recta: et novissima eius ducunt ad mortem.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 Anima laborantis laborat sibi, quia compulit eum os suum:
Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 Vir impius fodit malum, et in labiis eius ignis ardescit.
Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 Homo perversus suscitat lites: et verbosus separat principes.
Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 Vir iniquus lactat amicum suum: et ducit eum per viam non bonam.
Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 Qui attonitis oculis cogitat prava, mordens labia sua, perficit malum.
Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 Corona dignitatis senectus, quæ in viis iustitiæ reperietur.
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 Melior est patiens viro forti: et qui dominatur animo suo, expugnatore urbium.
Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
33 Sortes mittuntur in sinum, sed a Domino temperantur.
Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.

< Proverbiorum 16 >