< Proverbiorum 13 >

1 Filius sapiens, doctrina patris: qui autem illusor est, non audit cum arguitur.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 De fructu oris sui homo satiabitur bonis: anima autem prævaricatorum iniqua.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Qui custodit os suum, custodit animam suam: qui autem inconsideratus est ad loquendum, sentiet mala.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 Vult et non vult piger: anima autem operantium impinguabitur.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Verbum mendax iustus detestabitur: impius autem confundit, et confundetur.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 Iustitia custodit innocentis viam: impietas autem peccatorem supplantat.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Est quasi dives cum nihil habeat: et est quasi pauper, cum in multis divitiis sit.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 Redemptio animæ viri, divitiæ suæ: qui autem pauper est, increpationem non sustinet.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 Lux iustorum lætificat: lucerna autem impiorum extinguetur.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Inter superbos semper iurgia sunt: qui autem agunt omnia cum consilio, reguntur sapientia.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Substantia festinata minuetur: quæ autem paulatim colligitur manu, multiplicabitur.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 Spes, quæ differtur, affligit animam: lignum vitæ desiderium veniens.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Qui detrahit alicui rei, ipse se in futurum obligat: qui autem timet præceptum, in pace versabitur. Animæ dolosæ errant in peccatis: iusti autem misericordes sunt, et miserantur.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 Lex sapientis fons vitæ, ut declinet a ruina mortis.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Doctrina bona dabit gratiam: in itinere contemptorum vorago.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Astutus omnia agit cum consilio: qui autem fatuus est, aperit stultitiam.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Nuncius impii cadet in malum: legatus autem fidelis, sanitas.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Egestas, et ignominia ei, qui deserit disciplinam: qui autem acquiescit arguenti, glorificabitur.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Desiderium si compleatur, delectat animam: detestantur stulti eos, qui fugiunt mala.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 Qui cum sapientibus graditur, sapiens erit: amicus stultorum similis efficietur.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Peccatores persequitur malum: et iustis retribuentur bona.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 Bonus reliquit heredes filios, et nepotes: et custoditur iusto substantia peccatoris.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Multi cibi in novalibus patrum: et aliis congregantur absque iudicio.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Qui parcit virgæ, odit filium suum: qui autem diligit illum, instanter erudit.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Iustus comedit, et replet animam suam: venter autem impiorum insaturabilis.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

< Proverbiorum 13 >