< Mattheum 14 >

1 In illo tempore audivit Herodes tetrarcha fama Iesu:
Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.
2 et ait pueris suis: Hic est Ioannes Baptista: ipse surrexit a mortuis, et ideo virtutes operantur in eo.
Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”
3 Herodes enim tenuit Ioannem, et alligavit eum: et posuit in carcerem propter Herodiadem uxorem fratris sui.
Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.
4 Dicebat enim illi Ioannes: Non licet tibi habere eam.
Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”
5 Et volens illum occidere, timuit populum: quia sicut prophetam eum habebant.
Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.
6 Die autem natalis Herodis saltavit filia Herodiadis in medio, et placuit Herodi.
Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.
7 Unde cum iuramento pollicitus est ei dare quodcumque postulasset ab eo.
Katika kujibu kili aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.
8 At illa præmonita a matre sua, Da mihi, inquit, hic in disco caput Ioannis Baptistæ.
Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”
9 Et contristatus est rex: propter iuramentum autem, et eos, qui pariter recumbebant, iussit dari.
Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.
10 Misitque et decollavit Ioannem in carcere.
Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani
11 Et allatum est caput eius in disco, et datum est puellæ, et attulit matri suæ.
ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.
12 Et accedentes discipuli eius, tulerunt corpus eius, et sepelierunt illud: et venientes nunciaverunt Iesu.
Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.
13 Quod cum audisset Iesus, secessit inde in navicula, in locum desertum seorsum: et cum audissent turbæ, secutæ sunt eum pedestres de civitatibus.
Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.
14 Et exiens vidit turbam multam, et misertus est eis, et curavit languidos eorum.
Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.
15 Vespere autem facto, accesserunt ad eum discipuli eius, dicentes: Desertus est locus, et hora iam præteriit: dimitte turbas, ut euntes in castella, emant sibi escas.
Jioni ilipotimia, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.
16 Iesus autem dixit eis: Non habent necesse ire: date illis vos manducare.
Lakini Yesu akawaambia, ''Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”
17 Responderunt ei: Non habemus hic nisi quinque panes, et duos pisces.
Wakamwambia, ''Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”''
18 Qui ait eis: Afferte mihi illos huc.
Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”
19 Et cum iussisset turbam discumbere super fœnum, acceptis quinque panibus, et duobus piscibus, aspiciens in cælum benedixit, et fregit, et dedit discipulis panes, discipuli autem turbis.
Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini ya nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.
20 Et manducaverunt omnes, et saturati sunt. Et tulerunt reliquias, duodecim cophinos fragmentorum plenos.
Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.
21 Manducantium autem fuit numerus, quinque millia virorum, exceptis mulieribus, et parvulis.
Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.
22 Et statim compulit Iesus discipulos ascendere in naviculam, et præcedere eum trans fretum, donec dimitteret turbas.
Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.
23 Et dimissa turba, ascendit in montem solus orare. Vespere autem facto solus erat ibi.
Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.
24 Navicula autem in medio mari iactabatur fluctibus: erat enim contrarius ventus.
Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mpisho.
25 Quarta enim vigilia noctis, venit ad eos ambulans super mare.
Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.
26 Et videntes eum super mare ambulantem, turbati sunt, dicentes: Quia phantasma est. Et præ timore clamaverunt.
Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,'' na kupaaza sauti katika hali ya uoga.
27 Statimque Iesus locutus est eis, dicens: Habete fiduciam: ego sum, nolite timere.
Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! ni mimi! msiogope.”
28 Respondens autem Petrus dixit: Domine, si tu es, iube me ad te venire super aquas.
Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.''
29 At ipse ait: Veni. Et descendens Petrus de navicula, ambulabat super aquam ut veniret ad Iesum.
Yesu akasema, “Njoo.'' Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.
30 Videns vero ventum validum, timuit: et cum cœpisset mergi, clamavit dicens: Domine, salvum me fac.
Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!''
31 Et continuo Iesus extendens manum, apprehendit eum: et ait illi: Modicæ fidei, quare dubitasti?
Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”
32 Et cum ascendissent in naviculam, cessavit ventus.
Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulikoma kuvuma.
33 Qui autem in navicula erant, venerunt, et adoraverunt eum, dicentes: Vere, Filius Dei es.
Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”
34 Et cum transfretassent, venerunt in terram Genesar.
Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.
35 Et cum cognovissent eum viri loci illius, miserunt in universam regionem illam, et obtulerunt ei omnes male habentes:
Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.
36 et rogabant eum ut vel fimbriam vestimenti eius tangerent. Et quicumque tetigerunt, salvi facti sunt.
Walimsihi kwamba waweze kugusha pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.

< Mattheum 14 >