< Job 14 >

1 Homo natus de muliere, brevi vivens tempore, repletur multis miseriis.
Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
2 Qui quasi flos egreditur et conteritur, et fugit velut umbra, et numquam in eodem statu permanet.
Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
3 Et dignum ducis super huiuscemodi aperire oculos tuos, et adducere eum tecum in iudicium?
Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
4 Quis potest facere mundum de immundo conceptum semine? nonne tu qui solus es?
Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
5 Breves dies hominis sunt: numerus mensium eius apud te est: constituisti terminos eius, qui præteriri non poterunt.
Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
6 Recede paululum ab eo, ut quiescat, donec optata veniat, sicut mercenarii, dies eius.
Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
7 Lignum habet spem: si præcisum fuerit, rursum virescit, et rami eius pullulant.
Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
8 Si senuerit in terra radix eius, et in pulvere emortuus fuerit truncus illius,
Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
9 Ad odorem aquæ germinabit, et faciet comam quasi cum primum plantatum est:
hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
10 Homo vero cum mortuus fuerit, et nudatus atque consumptus, ubi quæso est?
Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
11 Quomodo si recedant aquæ de mari, et fluvius vacuefactus arescat:
Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
12 Sic homo cum dormierit, non resurget, donec atteratur cælum, non evigilabit, nec consurget de somno suo.
vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
13 Quis mihi hoc tribuat, ut in inferno protegas me, et abscondas me, donec pertranseat furor tuus, et constituas mihi tempus, in quo recorderis mei? (Sheol h7585)
Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
14 Putasne mortuus homo rursum vivat? cunctis diebus, quibus nunc milito, expecto donec veniat immutatio mea.
Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
15 Vocabis me, et ego respondebo tibi: operi manuum tuarum porriges dexteram.
Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
16 Tu quidem gressus meos dinumerasti, sed parce peccatis meis.
Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
17 Signasti quasi in sacculo delicta mea, sed curasti iniquitatem meam.
Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
18 Mons cadens defluit, et saxum transfertur de loco suo.
Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
19 Lapides excavant aquæ, et alluvione paulatim terra consumitur: et hominem ergo similiter perdes.
maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
20 Roborasti eum paululum ut in perpetuum transiret: immutabis faciem eius, et emittes eum.
Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
21 Sive nobiles fuerint filii eius, sive ignobiles, non intelliget.
Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
22 Attamen caro eius dum vivet dolebit, et anima illius super semetipso lugebit.
Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.

< Job 14 >