< Job 11 >

1 Respondens autem Sophar Naamathites, dixit:
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Numquid qui multa loquitur, non et audiet? aut vir verbosus iustificabitur?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Tibi soli tacebunt homines? et cum ceteros irriseris, a nullo confutaberis?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 Dixisti enim: Purus est sermo meus, et mundus sum in conspectu tuo.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 Atque utinam Deus loqueretur tecum, et aperiret labia sua tibi,
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 Ut ostenderet tibi secreta sapientiæ, et quod multiplex esset lex eius, et intelligeres quod multo minora exigaris ab eo, quam meretur iniquitas tua.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 Forsitan vestigia Dei comprehendes, et usque ad perfectum Omnipotentem reperies?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 Excelsior cælo est, et quid facies? profundior inferno, et unde cognosces? (Sheol h7585)
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 Longior terra mensura eius, et latior mari.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 Si subverterit omnia, vel in unum coarctaverit, quis contradicet ei?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 Ipse enim novit hominum vanitatem, et videns iniquitatem, nonne considerat?
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 Vir vanus in superbiam erigitur, et tamquam pullum onagri se liberum natum putat.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 Tu autem firmasti cor tuum, et expandisti ad eum manus tuas.
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 Si iniquitatem, quæ est in manu tua, abstuleris a te, et non manserit in tabernaculo tuo iniustitia:
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 Tunc levare poteris faciem tuam absque macula, et eris stabilis, et non timebis.
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 Miseriæ quoque oblivisceris, et quasi aquarum quæ præterierunt recordaberis.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Et quasi meridianus fulgor consurget tibi ad vesperam: et cum te consumptum putaveris, orieris ut lucifer.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 Et habebis fiduciam, proposita tibi spe, et defossus securus dormies.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Requiesces, et non erit qui te exterreat: et deprecabuntur faciem tuam plurimi.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 Oculi autem impiorum deficient, et effugium peribit ab eis, et spes illorum abominatio animæ.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >