< Genesis 10 >

1 Hæ sunt generationes filiorum Noe, Sem, Cham, et Iapheth: natique sunt eis filii post diluvium.
Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
2 Filii Iapheth: Gomer, et Magog, et Madai, et Iavan, et Thubal, et Mosoch, et Thiras.
Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
3 Porro filii Gomer: Ascenez et Riphath et Thogorma.
Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
4 Filii autem Iavan: Elisa et Tharsis, Cetthim et Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
5 Ab his divisæ sunt insulæ Gentium in regionibus suis, unusquisque secundum linguam suam et familias suas in nationibus suis.
Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
6 Filii autem Cham: Chus, et Mesraim, et Phuth, et Chanaan.
Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
7 Filii Chus: Saba, et Hevila, et Sabatha, et Regma, et Sabatacha. Filii Regma: Saba, et Dadan.
Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
8 Porro Chus genuit Nemrod: ipse cœpit esse potens in terra,
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
9 et erat robustus venator coram Domino. Ob hoc exivit proverbium: Quasi Nemrod robustus venator coram Domino.
Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
10 Fuit autem principium regni eius Babylon, et Arach, et Achad, et Chalanne, in terra Sennaar.
Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
11 De terra illa egressus est Assur, et ædificavit Niniven, et plateas civitatis, et Chale.
Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
12 Resen quoque inter Niniven et Chale: hæc est civitas magna.
na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
13 At vero Mesraim genuit Ludim, et Anamim, et Laabim, Nephthuim,
Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
14 et Phetrusim, et Chasluim: de quibus egressi sunt Philisthiim et Caphtorim.
Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
15 Chanaan autem genuit Sidonem primogenitum suum, Hethæum,
Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
16 et Iebusæum, et Amorrhæum, Gergesæum,
pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
17 Hevæum, et Aracæum: Sinæum,
Mhivi, Mwarki, Msini,
18 et Aradium, Samaræum et Amathæum: et post hæc disseminati sunt populi Chananæorum.
Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
19 Factique sunt termini Chanaan venientibus a Sidone Geraram usque Gazam, donec ingrediaris Sodomam et Gomorrham, et Adamam, et Seboim usque Lesa.
Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
20 Hi sunt filii Cham in cognationibus, et linguis, et generationibus, terrisque et gentibus suis.
Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
21 De Sem quoque nati sunt, patre omnium filiorum Heber, fratre Iapheth maiore.
Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
22 Filii Sem: Ælam et Assur, et Arphaxad, et Lud, et Aram.
Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
23 Filii Aram: Us, et Hul, et Gether, et Mes.
Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
24 At vero Arphaxad genuit Sale, de quo ortus est Heber.
Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
25 Natique sunt Heber filii duo: nomen uni Phaleg, eo quod in diebus eius divisa sit terra: et nomen fratris eius Iectan.
Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
26 Qui Iectan genuit Elmodad, et Saleph, et Asarmoth, Iare,
Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 et Aduram, et Uzal, et Decla,
Hadoram, Uzali, Dikla,
28 et Ebal, et Abimael, Saba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 et Ophir, et Hevila, et Iobab. Omnes isti, filii Iectan.
Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Et facta est habitatio eorum de Messa pergentibus usque Sephar montem orientalem.
Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
31 Isti filii Sem secundum cognationes et linguas, et regiones in gentibus suis.
Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
32 Hæ familiæ Noe iuxta populos et nationes suas. Ab his divisæ sunt gentes in terra post diluvium.
Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.

< Genesis 10 >