< 잠언 21 >

1 왕의 마음이 여호와의 손에 있음이 마치 보의 물과 같아서 그가 임의로 인도하시느니라
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 사람의 행위가 자기 보기에는 모두 정직하여도 여호와는 심령을 감찰하시느니라
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 의와 공평을 행하는 것은 제사 드리는 것보다 여호와께서 기쁘게 여기시느니라
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 눈이 높은 것과 마음이 교만한 것과 악인의 형통한 것은 다 죄니라
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 부지런한 자의 경영은 풍부함에 이를 것이나 조급한 자는 궁핍함에 이를 따름이니라
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 속이는 말로 재물을 모으는 것은 죽음을 구하는 것이라 곧 불려 다니는 안개니라
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 악인의 강포는 자기를 소멸하나니 이는 공의 행하기를 싫어함이니라
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 죄를 크게 범한 자의 길은 심히 구부러지고 깨끗한 자의 길은 곧으니라
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 다투는 여인과 함께 큰 집에서 나는 것보다 움막에서 혼자 사는 것이 나으니라
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 악인의 마음은 남의 재앙을 원하나니 그 이웃도 그 앞에서 은혜를 입지 못하느니라
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 거만한 자가 벌을 받으면 어리석은 자는 경성하겠고 지혜로운 자가 교훈을 받으면 지식이 더 하리라
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 의로우신 자는 악인의 집을 감찰하시고 악인을 환난에 던지시느니라
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 귀를 막아 가난한 자의 부르짖는 소리를 듣지 아니하면 자기의 부르짖을 때에도 들을 자가 없으리라
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 은밀한 선물은 노를 쉬게 하고 품의 뇌물은 맹렬한 분을 그치게 하느니라
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 공의를 행하는 것이 의인에게는 즐거움이요 죄인에게는 패망이니라
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 명철의 길을 떠난 사람은 사망의 회중에 거하리라
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 연락을 좋아하는 자는 가난하게 되고 술과 기름을 좋아하는 자는 부하게 되지 못하느니라
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 악인은 의인의 대속이 되고 궤사한 자는 정직한 자의 대신이 되느니라
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 다투며 성내는 여인과 함께 사는 것보다 광야에서 혼자 사는 것이 나으니라
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 지혜있는 자의 집에는 귀한 보배와 기름이 있으나 미련한 자는 이것을 다 삼켜버리느니라
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 의와 인자를 따라 구하는 자는 생명과 의와 영광을 얻느니라
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 지혜로운 자는 용사의 성에 올라가서 그 성의 견고히 의뢰하는 것을 파하느니라
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 입과 혀를 지키는 자는 그 영혼을 환난에서 보전하느니라
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 무례하고 교만한 자를 이름하여 망령된 자라 하나니 이는 넘치는 교만으로 행함이니라
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 게으른 자의 정욕이 그를 죽이나니 이는 그 손으로 일하기를 싫어 함이니라
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 어떤 자는 종일토록 탐하기만 하나 의인은 아끼지 아니하고 시제하느니라
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 악인의 제물은 본래 가증하거든 하물며 악한 뜻으로 드리는 것이랴
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 거짓 증인은 패망하려니와 확실한 증인의 말은 힘이 있느니라
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 악인은 그 얼굴을 굳게 하나 정직한 자는 그 행위를 삼가느니라
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 지혜로도 명철로도 모략으로도 여호와를 당치 못하느니라
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 싸울 날을 위하여 마병을 예비하거니와 이김은 여호와께 있느니라
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< 잠언 21 >