< 출애굽기 40 >

1 여호와께서 모세에게 일러 가라사대
Kisha Bwana akamwambia Mose:
2 너는 정월 초일일에 성막 곧 회막을 세우고
“Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
3 또 증거궤를 들여 놓고 또 장으로 그 궤를 가리우고
Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
4 또 상을 들여 놓고 그 위에 물품을 진설하고 등대를 들여 놓고 불을 켜고
Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
5 또 금 향단을 증거궤 앞에 두고 성막 문에 장을 달고
Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
6 또 번제단을 회막의 성막 문 앞에 놓고
“Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
7 또 물두멍을 회막과 단 사이에 놓고 그 속에 물을 담고
weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
8 또 뜰 주위에 포장을 치고 뜰 문에 장을 달고
Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
9 또 관유를 취하여 성막과 그 안에 있는 모든 것에 발라 그것과 그 모든 기구를 거룩하게 하라! 그것이 거룩하리라
“Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
10 너는 또 번제단과 그 모든 기구에 발라 그 안을 거룩하게 하라! 그 단이 지극히 거룩하리라
Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
11 너는 또 물두멍과 그 받침에 발라 거룩하게 하고
Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
12 또 아론과 그 아들들을 회막문으로 데려다가 물로 씻기고
“Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
13 아론에게 거룩한 옷을 입히고 그에게 기름을 부어 거룩하게 하여 그로 내게 제사장의 직분을 행하게 하라
Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 너는 또 그 아들들을 데려다가 그들에게 겉옷을 입히고
Walete wanawe na uwavike makoti.
15 그 아비에게 기름을 부음 같이 그들에게도 부어서 그들로 내게 제사장 직분을 행하게 하라 그들이 기름 부음을 받았은즉 대대로 영영히 제사장이 되리라 하시매
Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
16 모세가 그같이 행하되 곧 여호와께서 자기에게 명하신대로 다 행하였더라
Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
17 제 이년 정월 곧 그 달 초일일에 성막을 세우니라
Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
18 모세가 성막을 세우되, 그 받침들을 놓고 그 널판들을 세우고, 그 띠를 띠우고 그 기둥들을 세우고,
Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
19 또 성막 위에 막을 펴고 그 위에 덮개를 덮으니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
20 그가 또 증거판을 궤 속에 넣고 채를 궤에 꿰고 속죄소를 궤 위에 두고
Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
21 또 그 궤를 성막에 들여 놓고 장을 드리워서 그 증거궤를 가리우니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
22 그가 또 회막 안 곧 성막 북편으로 장 밖에 상을 놓고
Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
23 또 여호와 앞 그 상 위에 떡을 진설하니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
24 그가 또 회막 안 곧 성막 남편에 등대를 놓아 상과 대하게 하고
Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
25 또 여호와 앞에 등잔에 불을 켜니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
26 그가 또 금 향단을 회막 안 장 앞에 두고
Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
27 그 위에 향기로운 향을 사르니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
28 그가 또 성막문에 장을 달고
Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
29 또 회막의 성막 문 앞에 번제단을 두고 번제와 소제를 그 위에 드리니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
30 그가 또 물두멍을 회막과 단 사이에 두고 거기 씻을 물을 담고
Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
31 자기와 아론과 그 아들들이 거기서 수족을 씻되
Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
32 그들이 회막에 들어갈 때와 단에 가까이 갈 때에 씻었으니 여호와께서 모세에게 명하신 대로 되니라
Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
33 그가 또 성막과 단 사면 뜰에 포장을 치고 뜰문의 장을 다니라 모세가 이같이 역사를 필하였더라
Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
34 그 후에 구름이 회막에 덮이고 여호와의 영광이 성막에 충만하매
Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
35 모세가 회막에 들어갈 수 없었으니 이는 구름이 회막 위에 덮이고 여호와의 영광이 성막에 충만함이었으며
Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
36 구름이 성막 위에서 떠오를 때에는 이스라엘 자손이 그 모든 행하는 길에 앞으로 발행하였고
Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
37 구름이 떠오르지 않을 때에는 떠오르는 날까지 발행하지 아니하였으며
lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
38 낮에는 여호와의 구름이 성막 위에 있고 밤에는 불이 그 구름 가운데 있음을 이스라엘의 온 족속이 그 모든 행하는 길에서 친히 보았더라
Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.

< 출애굽기 40 >