< マタイの福音書 24 >

1 第三項 イエズスエルザレムの滅亡等を豫言し給ふ イエズス[神]殿を出でて往き給ひけるに、弟子等[神]殿の構造を示さんとて近づきしかば、
Yesu alitoka Hekaluni, na alipokuwa akienda zake, wanafunzi wake walimwendea, wakamwonyesha majengo ya Hekalu.
2 答へて曰ひけるは、汝等此一切の物を見るか、我誠に汝等に告ぐ、此處には一の石も崩れずして石の上に遺されじ、と。
Yesu akawaambia, “Sawa, mnaweza kuyatazama haya yote! Kweli nawaambieni, hakuna hata jiwe moja litakalosalia hapa juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
3 斯て橄欖山に坐し給へるに、弟子等竊に近づきて云ひけるは、此事等のあらんは何時なるぞ、又汝の再臨と世の終との兆は何なるぞ。 (aiōn g165)
Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni, wanafunzi walimwendea faraghani, wakamwuliza, “Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kuja kwako na mwisho wa nyakati?” (aiōn g165)
4 イエズス答へて曰ひけるは、汝等人に惑はされじと注意せよ、
Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
5 其は多くの人我名を冒し來りて、我はキリストなりと云ひて、多くの人を惑はすべければなり。
Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye Kristo, nao watawapotosha watu wengi.
6 即汝等戰闘と戰闘の風説を聞かん、而も慎みて心を騒がす事勿れ、是等の事蓋あるべし、然れど終は未至らざるなり。
Mtasikia juu ya vita na fununu za vita; lakini msifadhaike, maana hayo hayana budi kutokea, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
7 即民は民に、國は國に立逆らひ、又疫病飢饉地震處々にあらん、
Taifa moja litapigana na taifa lingine; ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine. Hapa na pale patakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi.
8 是皆苦の初なり。
Yote hayo ni kama mwanzo wa maumivu ya kujifungua mtoto.
9 其時人々汝等を困難に陥入れ、又死に處し、汝等我名の為に萬民に憎まれん。
“Kisha watawatoeni ili mteswe na kuuawa. Mataifa yote yatawachukieni kwa ajili ya jina langu.
10 其時多くの人躓きて、互に反應し互に憎み、
Tena, wengi wataiacha imani yao, watasalitiana na kuchukiana.
11 又僞預言者多く起りて、多くの人を惑はさん、
Watatokea manabii wengi wa uongo watakaowapotosha watu wengi.
12 且不義の溢れたるによりて、多數の人の愛冷えん、
Kwa sababu ya ongezeko la uhalifu, upendo wa watu wengi utafifia.
13 然れど終まで耐忍ぶ人は救はるべし。
Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokoka.
14 [天]國の此福音は、萬民に證として全世界に宣傳へられん、斯て後終は至るべし。
Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.
15 然れば汝等、預言者ダニエルに託りて告げられし「最憎むべき荒廃」が聖所に厳然たるを見ば、
“Basi, mtakapoona Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),
16 読む人悟るべし。其時ユデアに居る人は山に遁るべし、
hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.
17 屋根に居る人は、其家より何物をか取出ださんとて下るべからず、
Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.
18 畑に居る人は、其上着を取らんとて歸るべからず。
Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
19 其日に當りて懐胎せる人、乳を哺まする人は禍なる哉。
Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
20 汝等の遁ぐる事の、或は冬、或は安息日に當らざらん事を祈れ。
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!
21 其時には、世の始より曾て無く、又後にも有るまじき程の、大なる患難あるべければなり。
Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.
22 其日若縮められずば、救はるる人なからん、然れど其日は、選まれたる人々の為に縮めらるべし。
Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.
23 其時若人ありて汝等に、「看よキリストは此處に在り、彼處に在り」と云ふとも信ずること勿れ、
“Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: Kristo yuko hapa au Yuko pale, msimsadiki.
24 其は僞キリスト及僞預言者起りて、大なる徴と奇蹟とを行ひ、能ふべくんば選まれたる人々をさへも惑はさんとすべければなり。
Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.
25 我預之を汝等に告げたるぞ。然れば汝等假令、「看よキリストは荒野に在り」と云はるとも出ること勿れ、
Sikilizeni, nimekwisha kuwaonya kabla ya wakati.
26 「看よ奥室に在り」と云はるとも信ずること勿れ、
Basi, wakiwaambieni, Tazameni, yuko jangwani, msiende huko; au, Tazameni, amejificha ndani, msisadiki;
27 其は電光の東より出て西にまで見ゆる如く、人の子の來るも亦然るべければなり。
maana, kama vile umeme uangazavyo toka mashariki hadi magharibi, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
28 総て屍の在る處には鷲も亦集らん。
Pale ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29 此日々の患難の後、直に日晦み、月其光を與へず、星天より隕ち、天の能力総て動揺せん。
“Mara baada ya dhiki ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
30 其時人の子の徴空に現れん。其時又地の民族悉く哭き、人の子が大なる能力と威光とを以て空の雲に乗り來るを見ん。
Kisha, ishara ya Mwana wa Mtu itaonekana angani, na hapo makabila yote duniani yatalalamika; watamwona Mwana wa Mtu akija juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi.
31 彼聲高き喇叭を持てる己が天使等を遣はし、天の此涯まで、四方より其選まれし人々を集めしめん。
Naye atawatuma malaika wake wenye tarumbeta la kuvuma sana, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, toka mwisho huu wa mbingu hadi mwisho huu.
32 汝等無花果樹より喩を學べ、其枝既に柔ぎて葉の生ずる時、汝等は夏の近きを知る。
“Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33 斯の如く、此一切の事を見ば、既に門に近しと知れ。
Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo haya yote yakitendeka, jueni kwamba yuko karibu sana.
34 我誠に汝等に告ぐ、是等の事の皆成る迄は、現代は過ぎざらん。
Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
35 天地は過ぎん、然れど我言は過ぎざるべし。
Naam, mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 其日其時をば何人も知らず、天使すらも知らず、知り給へるは唯父獨のみ。
“Lakini, juu ya siku au saa hiyo, hakuna mtu ajuaye itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake ndiye ajuaye.
37 ノエの日に於る如く、人の子の來るも亦然らん。
Kwa maana kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Mtu.
38 即洪水の前の頃、ノエの方舟に入る其日までも、人々飲み食ひ娶り嫁ぎして、
Maana nyakati hizo, kabla ya gharika kuu, watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka Noa alipoingia ndani ya ile safina.
39 洪水來りて悉く彼等を引浚ふまで知らざりし如く、人の子の來るも亦然らん。
Hawakujua kuna nini mpaka ile gharika ilipotokea, ikawakumba wote. Ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mtu atakapokuja.
40 其時二人畑に在らんに、一人は取られ一人は遺されん。
Wakati huo watu wawili watakuwa shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
41 二人の女磨を挽き居らんに、一人は取られ一人は遺されん。
Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.
42 然れば汝等警戒せよ、汝等の主の來り給ふは何れの時なるかを知らざればなり。
Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.
43 汝等之を知れ、家父若盗賊の來るべき時を知らば、必警戒して其家を穿たせじ。
Lakini kumbukeni jambo hili: kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
44 然れば汝等も用意してあれ、汝等の知らざる時に人の子來るべければなり。
Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
45 時に應じて糧を其僕等に與へさせんとて、主人が彼等の上に立てたる、忠誠怜悧なる僕を誰と思ふぞ。
Yesu akaendelea kusema, “Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?
46 其主人の來らん時、然するを見出されたる僕は福なり。
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47 我誠に汝等に告ぐ、主人は其凡ての所有を是に宰らしめん。
Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48 然れど若彼惡しき僕、心の中に「主人の來ること遅し」と謂ひて、
Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: Bwana wangu anakawia kurudi,
49 其同輩に殴掛り、酒徒と酒食を共にせば、
kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50 其僕の主人、彼が思はざる日、知らざる時に來りて、
bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51 之を處罰し、其報を僞善者と同じうすべし、其處には痛哭と切歯とあらん。
Atamkatilia mbali na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.

< マタイの福音書 24 >