< エペソ人への手紙 6 >

1 子たる者よ、主に於て汝等の父母に從へ、蓋是正當の事なり。
Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2 「汝の父母を敬へ」とは、約束を附したる第一の掟にして、
“Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3 即ち「汝が福を得て地上に長命ならん為」となり。
“Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
4 父たる者よ、汝等も其子等の怒を買ふ事なくして、主の規律と訓戒との中に之を育てよ。
Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5 奴隷たる者よ、キリストに從ふが如くに畏れ慄き、単純なる心を以て肉身上の主人に順へ。
Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6 人々の意に適はんとするが如くに目前のみにて事へず、キリストの奴隷として心より神の思召を為し、
Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7 事ふる事、人に於てせず主に於てするが如くに、快くせよ。
Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8 其は奴隷たると自由の身たるとを問はず、各自の為したる善は、何れも主より報いらるべしと知ればなり。
Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9 主人たる者よ、汝等も亦奴隷に對ひて為す事斯の如くにして、彼等に威嚇を加ふること勿れ、其は彼等と汝等との主天に在して、人に就きて偏り給ふ事なしと知ればなり。
Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10 第四項 信者は雄々しく信仰の為に戰ふべし 終に臨みて、兄弟等よ、汝等主に於て又其大能の勢力に於て氣力を得、
Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11 惡魔の計畧に勝つことを得ん為に、神の武具を身に着けよ。
Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12 其は我等の戰ふべきは血肉に對ひてには非ず、権勢及び能力、此暗黒の世の司等、天空の惡霊等に對ひてなればなり。 (aiōn g165)
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn g165)
13 然れば惡き日に抵抗し、萬事に成功して立つ事を得ん為に、神の武具を執れ。
Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14 然れば起て汝等、腰に眞實を帯し、身に正義の鎧を着け、
Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15 足に平和の福音に對する奮發を履き、
na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16 凡ての場合に於て惡魔の火箭を消すべき信仰の楯を執り、
Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17 救霊の兜と神の御言なる[聖]霊の剣を執り、
Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18 尚且凡て祈祷及び懇願を以て、何れの機會に於ても聖霊に由りて祈り、忍耐を以て聖徒一同の為に懇願する事に注意せよ。
Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19 又我為にも然なして、我は福音の奥義の為に鎖に繋がれたる使節なれば、憚らず口を開きて之を知らする様、言を賜はり、
Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20 之に就きて我が語るべき儘に敢て語る様に祈れ。
Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21 結末 我に関する事、我為す事を汝等も知らん為に、我至愛なる兄弟にして主の忠實なる役者たるチキコは、萬事を汝等に告ぐるならん。
Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22 我が彼を遣はししは之が為、即ち彼が我等に関する事を汝等に知らせて、汝等の心を慰めん為なり。
Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23 願はくは父にて在す神、及び主イエズス、キリストより、平安と愛と信仰とを兄弟等に賜はらん事を。
Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24 願はくは我主イエズス、キリストを變らず愛し奉る凡ての人に恩寵あらん事を、アメン。
Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.

< エペソ人への手紙 6 >