< エペソ人への手紙 6 >

1 子たる者よ、主に於て汝等の父母に從へ、蓋是正當の事なり。
Watoto watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa maana hii ni haki.
2 「汝の父母を敬へ」とは、約束を附したる第一の掟にして、
“Mheshimu baba yako na mama yako” (Maana hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi),
3 即ち「汝が福を得て地上に長命ならん為」となり。
“ili iwe heri kwenu na muweze kuishi maisha marefu juu ya nchi.”
4 父たる者よ、汝等も其子等の怒を買ふ事なくして、主の規律と訓戒との中に之を育てよ。
Na ninyi akina baba, msiwakwaze watoto na kuwasababishia hasira, badala yake, waleeni katika maonyo na maagizo ya Bwana.
5 奴隷たる者よ、キリストに從ふが如くに畏れ慄き、単純なる心を以て肉身上の主人に順へ。
Enyi watumwa, iweni watiifu kwa mabwana zenu wa hapa duniani kwa heshima kubwa na kutetemeka kwa hofu itokayo mioyoni mwenu. muwe watiifu kwao kama vile mnavyomtii Kristo.
6 人々の意に適はんとするが如くに目前のみにて事へず、キリストの奴隷として心より神の思召を為し、
Utii wenu usiwe tu pale mabwana zenu wanapowatazama ili kuwafurahisha. Badala yake, iweni watiifu kama watumwa wa Kristo. Fanyeni Mapenzi ya Mungu kutoka mioyoni mwenu,
7 事ふる事、人に於てせず主に於てするが如くに、快くせよ。
watumikieni kwa mioyo yenu yote, kwa kuwa mnamtumikia Bwana na wala si wanadamu,
8 其は奴隷たると自由の身たるとを問はず、各自の為したる善は、何れも主より報いらるべしと知ればなり。
mnapaswa kujua kwamba katika kila tendo jema mtu analofanya, atapokea zawadi kutoka kwa Bwana, ikiwa ni mtumwa au mtu huru.
9 主人たる者よ、汝等も亦奴隷に對ひて為す事斯の如くにして、彼等に威嚇を加ふること勿れ、其は彼等と汝等との主天に在して、人に就きて偏り給ふ事なしと知ればなり。
Na ninyi mabwana fanyeni vivyo hivyo kwa watumwa wenu. Msiwatishe mkijua kwamba yeye aliye Bwana wa wote ni yule aliye mbinguni. Mkijua kuwa hakuna upendeleo ndani yake.
10 第四項 信者は雄々しく信仰の為に戰ふべし 終に臨みて、兄弟等よ、汝等主に於て又其大能の勢力に於て氣力を得、
Hatimaye, iweni na nguvu katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake.
11 惡魔の計畧に勝つことを得ん為に、神の武具を身に着けよ。
Vaeni silaha zote za Mungu, ili kwamba mpate kusimama kinyume na hila za shetani.
12 其は我等の戰ふべきは血肉に對ひてには非ず、権勢及び能力、此暗黒の世の司等、天空の惡霊等に對ひてなればなり。 (aiōn g165)
kwa kuwa vita yetu si ya damu na nyama, bali ni dhidi ya falme na mamlaka ya roho na watawala wa ulimwengu wa uovu na giza, dhidi ya pepo katika sehemu za mbingu. (aiōn g165)
13 然れば惡き日に抵抗し、萬事に成功して立つ事を得ん為に、神の武具を執れ。
Kwa hiyo, vaeni silaha zote za Mungu, ili mpate kusimama imara dhidi ya uovu katika kipindi hiki kiovu. Baada ya kumaliza kila kitu, mtasimama imara.
14 然れば起て汝等、腰に眞實を帯し、身に正義の鎧を着け、
Hatimaye simameni imara. Fanyeni hivi baada ya kuwa mmefunga mkanda katika kweli na haki kifuani.
15 足に平和の福音に對する奮發を履き、
Fanyini hivi mkiwa mmevaa utayari miguuni mwenu wa kutangaza injili ya amani.
16 凡ての場合に於て惡魔の火箭を消すべき信仰の楯を執り、
Katika kila hali mkichukua ngao ya imani, ambayo itakuwezesha kuizima mishale ya yule mwovu.
17 救霊の兜と神の御言なる[聖]霊の剣を執り、
Vaeni kofia ya wokovu na upanga wa Roho, ambayo ni neno la Mungu.
18 尚且凡て祈祷及び懇願を以て、何れの機會に於ても聖霊に由りて祈り、忍耐を以て聖徒一同の為に懇願する事に注意せよ。
pamoja na maombi na dua. Ombeni kwa Roho kila wakati. Kwa mtazamo huu iweni waangalifu kila wakati kwa uvumilivu wote na maombi kwa ajili ya waamini wote.
19 又我為にも然なして、我は福音の奥義の為に鎖に繋がれたる使節なれば、憚らず口を開きて之を知らする様、言を賜はり、
Ombeni kwa ajili yangu, ili nipewe ujumbe ninapofungua mdomo wangu. Ombeni kwamba nieleweshe kwa ujasiri kweli iliyofichika ihusuyo injili.
20 之に就きて我が語るべき儘に敢て語る様に祈れ。
Ni kwa ajili ya injili mimi ni balozi niliyefungwa minyororo, ili kwamba ndani mwao niseme kwa ujasiri kama ninavyowiwa kusema.
21 結末 我に関する事、我為す事を汝等も知らん為に、我至愛なる兄弟にして主の忠實なる役者たるチキコは、萬事を汝等に告ぐるならん。
Lakini ninyi pia mjue mambo yangu na jinsi ninavyoendelea, Tikiko ndugu yangu kipenzi na mtumishi mwaminifu katika Bwana, atawajulisha kila kitu.
22 我が彼を遣はししは之が為、即ち彼が我等に関する事を汝等に知らせて、汝等の心を慰めん為なり。
Nimemtuma kwenu kwa kusudi hili maalumu, ili kwamba mjue mambo kuhusu sisi, aweze kuwafariji mioyo yenu.
23 願はくは父にて在す神、及び主イエズス、キリストより、平安と愛と信仰とを兄弟等に賜はらん事を。
Amani na iwe kwa ndugu, na upendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu baba na Bwana Yesu Kristo.
24 願はくは我主イエズス、キリストを變らず愛し奉る凡ての人に恩寵あらん事を、アメン。
Neema na iwe pamoja na wote wanampenda Bwana Yesu Kristo kwa pendo lile lisilo kufa.

< エペソ人への手紙 6 >