< 詩篇 95 >

1 さあ、われらは主にむかって歌い、われらの救の岩にむかって喜ばしい声をあげよう。
Oh njoni, tumwimbie Yahwe; na tumwimbie kwa shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2 われらは感謝をもって、み前に行き、主にむかい、さんびの歌をもって、喜ばしい声をあげよう。
Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
3 主は大いなる神、すべての神にまさって大いなる王だからである。
Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4 地の深い所は主のみ手にあり、山々の頂もまた主のものである。
Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
5 海は主のもの、主はこれを造られた。またそのみ手はかわいた地を造られた。
Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.
6 さあ、われらは拝み、ひれ伏し、われらの造り主、主のみ前にひざまずこう。
Oh njoni, tumwabudu na tupige magoti; tupige magoti mbele za Yahwe, muumbaji wetu:
7 主はわれらの神であり、われらはその牧の民、そのみ手の羊である。どうか、あなたがたは、きょう、そのみ声を聞くように。
Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tu watu wa malisho yake na kondoo wa mkono wake. Ni heri leo mngesikia sauti yake!
8 あなたがたは、メリバにいた時のように、また荒野のマッサにいた日のように、心をかたくなにしてはならない。
Msiifanye migumu mioyo yenu, kama vile huko Meriba, au kama ile siku ya Masa jangwani,
9 あの時、あなたがたの先祖たちはわたしのわざを見たにもかかわらず、わたしを試み、わたしをためした。
ambako baba zenu walinijaribu na kunipima, japo walikuwa wameyaona matendo yangu.
10 わたしは四十年の間、その代をきらって言った、「彼らは心の誤っている民であって、わたしの道を知らない」と。
Kwa miaka arobaini nilikasirishwa na kizazi hicho na kusema, 'Hawa ni watu ambao mioyo yao imepotoka; hawazijui njia zangu.'
11 それゆえ、わたしは憤って、彼らはわが安息に入ることができないと誓った。
Hivyo katika hasira yangu niliapa kwamba wasingeingia kamwe mahali pa pumziko.”

< 詩篇 95 >