< 詩篇 91 >

1 いと高き者のもとにある隠れ場に住む人、全能者の陰にやどる人は
Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
2 主に言うであろう、「わが避け所、わが城、わが信頼しまつるわが神」と。
Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
3 主はあなたをかりゅうどのわなと、恐ろしい疫病から助け出されるからである。
Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
4 主はその羽をもって、あなたをおおわれる。あなたはその翼の下に避け所を得るであろう。そのまことは大盾、また小盾である。
Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
5 あなたは夜の恐ろしい物をも、昼に飛んでくる矢をも恐れることはない。
Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
6 また暗やみに歩きまわる疫病をも、真昼に荒す滅びをも恐れることはない。
wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
7 たとい千人はあなたのかたわらに倒れ、万人はあなたの右に倒れても、その災はあなたに近づくことはない。
Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
8 あなたはただ、その目をもって見、悪しき者の報いを見るだけである。
Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
9 あなたは主を避け所とし、いと高き者をすまいとしたので、
Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
10 災はあなたに臨まず、悩みはあなたの天幕に近づくことはない。
Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
11 これは主があなたのために天使たちに命じて、あなたの歩むすべての道であなたを守らせられるからである。
Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
12 彼らはその手で、あなたをささえ、石に足を打ちつけることのないようにする。
Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
13 あなたはししと、まむしとを踏み、若いししと、へびとを足の下に踏みにじるであろう。
Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
14 彼はわたしを愛して離れないゆえに、わたしは彼を助けよう。彼はわが名を知るゆえに、わたしは彼を守る。
Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
15 彼がわたしを呼ぶとき、わたしは彼に答える。わたしは彼の悩みのときに、共にいて、彼を救い、彼に光栄を与えよう。
Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
16 わたしは長寿をもって彼を満ち足らせ、わが救を彼に示すであろう。
Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.

< 詩篇 91 >