< 詩篇 80 >

1 聖歌隊の指揮者によってゆりの花のしらべにあわせてうたわせたアサフのあかしの歌 イスラエルの牧者よ、羊の群れのようにヨセフを導かれる者よ、耳を傾けてください。ケルビムの上に座せられる者よ、光を放ってください。
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 エフライム、ベニヤミン、マナセの前にあなたの力を振り起し、来て、われらをお救いください。
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 神よ、われらをもとに返し、み顔の光を照してください。そうすればわれらは救をえるでしょう。
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 万軍の神、主よ、いつまで、その民の祈にむかってお怒りになるのですか。
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 あなたは涙のパンを彼らに食わせ、多くの涙を彼らに飲ませられました。
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 あなたはわれらを隣り人のあざけりとし、われらの敵はたがいにあざわらいました。
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 万軍の神よ、われらをもとに返し、われらの救われるため、み顔の光を照してください。
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 あなたは、ぶどうの木をエジプトから携え出し、もろもろの国民を追い出して、これを植えられました。
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 あなたはこれがために地を開かれたので、深く根ざして、国にはびこりました。
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 山々はその影でおおわれ、神の香柏はその枝でおおわれました。
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 これはその枝を海にまでのべ、その若枝を大川にまでのべました。
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 あなたは何ゆえ、そのかきをくずして道ゆくすべての人にその実を摘み取らせられるのですか。
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 林のいのししはこれを荒し、野のすべての獣はこれを食べます。
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 万軍の神よ、再び天から見おろして、このぶどうの木をかえりみてください。
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 あなたの右の手の植えられた幹と、みずからのために強くされた枝とをかえりみてください。
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 彼らは火をもってこれを焼き、これを切り倒しました。彼らをみ顔のとがめによって滅ぼしてください。
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 しかしあなたの手をその右の手の人の上におき、みずからのために強くされた人の子の上においてください。
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 そうすれば、われらはあなたを離れ退くことはありません。われらを生かしてください。われらはあなたのみ名を呼びます。
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 万軍の神、主よ、われらをもとに返し、み顔の光を照してください。そうすればわれらは救をえるでしょう。
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< 詩篇 80 >