< 詩篇 51 >

1 聖歌隊の指揮者によってうたわせたダビデの歌、これはダビデがバテセバに通った後預言者ナタンがきたときによんだもの 神よ、あなたのいつくしみによって、わたしをあわれみ、あなたの豊かなあわれみによって、わたしのもろもろのとがをぬぐい去ってください。
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba. Ee Mungu, unihurumie, kwa kadiri ya upendo wako usiokoma, kwa kadiri ya huruma yako kuu, uyafute makosa yangu.
2 わたしの不義をことごとく洗い去り、わたしの罪からわたしを清めてください。
Unioshe na uovu wangu wote na unitakase dhambi yangu.
3 わたしは自分のとがを知っています。わたしの罪はいつもわたしの前にあります。
Kwa maana ninajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 わたしはあなたにむかい、ただあなたに罪を犯し、あなたの前に悪い事を行いました。それゆえ、あなたが宣告をお与えになるときは正しく、あなたが人をさばかれるときは誤りがありません。
Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 見よ、わたしは不義のなかに生れました。わたしの母は罪のうちにわたしをみごもりました。
Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 見よ、あなたは真実を心のうちに求められます。それゆえ、わたしの隠れた心に知恵を教えてください。
Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni, ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
7 ヒソプをもって、わたしを清めてください、わたしは清くなるでしょう。わたしを洗ってください、わたしは雪よりも白くなるでしょう。
Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi, unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 わたしに喜びと楽しみとを満たし、あなたが砕いた骨を喜ばせてください。
Unipe kusikia furaha na shangwe, mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 み顔をわたしの罪から隠し、わたしの不義をことごとくぬぐい去ってください。
Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu, na uufute uovu wangu wote.
10 神よ、わたしのために清い心をつくり、わたしのうちに新しい、正しい霊を与えてください。
Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.
11 わたしをみ前から捨てないでください。あなたの聖なる霊をわたしから取らないでください。
Usinitupe kutoka mbele zako wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.
12 あなたの救の喜びをわたしに返し、自由の霊をもって、わたしをささえてください。
Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, unipe roho ya utii, ili initegemeze.
13 そうすればわたしは、とがを犯した者にあなたの道を教え、罪びとはあなたに帰ってくるでしょう。
Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14 神よ、わが救の神よ、血を流した罪からわたしを助け出してください。わたしの舌は声高らかにあなたの義を歌うでしょう。
Ee Mungu, Mungu uniokoaye, niokoe na hatia ya kumwaga damu, nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako.
15 主よ、わたしのくちびるを開いてください。わたしの口はあなたの誉をあらわすでしょう。
Ee Bwana, fungua midomo yangu, na kinywa changu kitatangaza sifa zako.
16 あなたはいけにえを好まれません。たといわたしが燔祭をささげてもあなたは喜ばれないでしょう。
Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta, hufurahii sadaka za kuteketezwa.
17 神の受けられるいけにえは砕けた魂です。神よ、あなたは砕けた悔いた心をかろしめられません。
Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika, moyo uliovunjika wenye toba, Ee Mungu, hutaudharau.
18 あなたのみこころにしたがってシオンに恵みを施し、エルサレムの城壁を築きなおしてください。
Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi, ukazijenge upya kuta za Yerusalemu.
19 その時あなたは義のいけにえと燔祭と、全き燔祭とを喜ばれるでしょう。その時あなたの祭壇に雄牛がささげられるでしょう。
Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki, sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana, pia mafahali watatolewa madhabahuni mwako.

< 詩篇 51 >