< 詩篇 33 >

1 正しき者よ、主によって喜べ、さんびは直き者にふさわしい。
Furahini katika Yahwe, ninyi wenye haki; kusifu kwa wenye haki kwa faa sana.
2 琴をもって主をさんびせよ、十弦の立琴をもって主をほめたたえよ。
Mshukuruni Bwana kwa kinubi; mwimbieni sifa kwa kinubi chenye nyuzi kumi.
3 新しい歌を主にむかって歌い、喜びの声をあげて巧みに琴をかきならせ。
Mwimbieni yeye wimbo mpaya; pigeni kwa ustadi na muimbe kwa furaha.
4 主のみことばは直く、そのすべてのみわざは真実だからである。
Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
5 主は正義と公平とを愛される。地は主のいつくしみで満ちている。
Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
6 もろもろの天は主のみことばによって造られ、天の万軍は主の口の息によって造られた。
Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
7 主は海の水を水がめの中に集めるように集め、深い淵を倉におさめられた。
Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
8 全地は主を恐れ、世に住むすべての者は主を恐れかしこめ。
Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
9 主が仰せられると、そのようになり、命じられると、堅く立ったからである。
Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.
10 主はもろもろの国のはかりごとをむなしくし、もろもろの民の企てをくじかれる。
Yahwe huvunja muungano wa mataifa; naye huishinda mipango ya wanadamu.
11 主のはかりごとはとこしえに立ち、そのみこころの思いは世々に立つ。
Mipango ya Yahwe husimama milele, mipango ya moyo wake ni kwa ajili ya vizazi vyote.
12 主をおのが神とする国はさいわいである。主がその嗣業として選ばれた民はさいわいである。
Limebarikiwa taifa ambalo Mungu wao ni Yahwe, watu ambao yeye amewachagua kama warithi wake.
13 主は天から見おろされ、すべての人の子らを見、
Yahwe anatazama kutoka mbinguni; yeye huona watu wote.
14 そのおられる所から地に住むすべての人をながめられる。
Kutokea mahali ambapo yeye anaishi, huwatazama wote waishio juu ya nchi.
15 主はすべて彼らの心を造り、そのすべてのわざに心をとめられる。
Yeye anaye iumba mioyo yao na kuyaona matendo yao yote.
16 王はその軍勢の多きによって救を得ない。勇士はその力の大いなるによって助けを得ない。
Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa; shujaa haokolewi na nguvu zake nyingi.
17 馬は勝利に頼みとならない。その大いなる力も人を助けることはできない。
Farasi sio salama kwa ajili ya ushindi; ijapokuwa nguvu zake ni nyingi, hawezi kuokoa.
18 見よ、主の目は主を恐れる者の上にあり、そのいつくしみを望む者の上にある。
Tazama, macho ya Yahwe yako kwa wale wanao mhofu yeye, wale wanao litumainia agano lake takatifu
19 これは主が彼らの魂を死から救い、ききんの時にも生きながらえさせるためである。
kuwaokoa maisha yao na mauti na kuwaweka hai wakati wa jaa.
20 われらの魂は主を待ち望む。主はわれらの助け、われらの盾である。
Sisi tunamngoja Yahwe, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 われらは主の聖なるみ名に信頼するがゆえに、われらの心は主にあって喜ぶ。
Mioyo yetu hufurahia ndani yake, kwa kuwa tunaamini katika jina lake takatifu.
22 主よ、われらが待ち望むように、あなたのいつくしみをわれらの上にたれてください。
Yahwe, agano lako takatifu, liwe pamoja nasi tuwekapo tumaini letu katika wewe.

< 詩篇 33 >