< 詩篇 139 >

1 伶長にうたはしめたるダビデの歌 ヱホバよなんぢは我をさぐり我をしりたまへり
Ee Yahwe, wewe umenichunguza, na unanijua.
2 なんぢはわが坐るをも立をもしり 又とほくよりわが念をわきまへたまふ
Wewe unajua nikaapo na niinukapo; unayajua mawazo yangu tokea mbali sana.
3 なんぢはわが歩むをもわが臥をもさぐりいだし わがもろもろの途をことごとく知たまへり
Unachunguza wenendo wangu na kulala kwangu; unazijua njia zangu zote.
4 そはわが舌に一言ありとも観よヱホバよなんぢことごとく知たまふ
Kabla hakujawa na neno kwenye ulimi wangu, wewe unalijua kabisa, Yahwe.
5 なんぢは前より後よりわれをかこみ わが上にその手をおき給へり
Nyuma yangu na mbele yangu unanizunguka na kuniwekea mkono wako.
6 かかる知識はいとくすしくして我にすぐ また高くして及ぶことあたはず
Maarifa hayo ni mengi yananizidi mimi; yako juu sana, nami siwezi kuyafikia.
7 我いづこにゆきてなんぢの聖霊をはなれんや われいづこに往てなんぢの前をのがれんや
Niende wapi mbali na roho yako? Niende wapi niukimbie uwepo wako?
8 われ天にのぼるとも汝かしこにいまし われわが榻を陰府にまうくるとも 観よなんぢ彼處にいます (Sheol h7585)
Kama nikipaa mbinguni, uko huko; kama nikifanya kitanda changu Kuzimuni, tazama, uko huko. (Sheol h7585)
9 我あけぼのの翼をかりて海のはてにすむとも
Kama nikipaa kwa mbawa za asubuhi na kwenda kuishi pande za mwisho wa bahari,
10 かしこにて尚なんぢの手われをみちびき汝のみぎの手われをたもちたまはん
hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika.
11 暗はかならす我をおほひ 我をかこめる光は夜とならんと我いふとも
Kama nikisema, “Hakika giza litanifunika, na nuru inizungukayo itakuwa usiku,”
12 汝のみまへには暗ものをかくすことなく 夜もひるのごとくに輝けり なんぢにはくらきも光もことなることなし
Hata giza lisingweza kuwa giza kwako. Usiku ungeng'aa kama mchana, maana giza na nuru kwako vinafanana.
13 汝はわがはらわたをつくり 又わがははの胎にわれを組成たまひたり
Wewe uliumba sehemu zangu za ndani; uliniumba tumboni mwa mama yangu.
14 われなんぢに感謝す われは畏るべく奇しくつくられたり なんぢの事跡はことごとくくすし わが霊魂はいとつばらに之をしれり
Nitakusifu, kwa maana nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu. Nafsi yangu yalijua hili vizuri sana.
15 われ隠れたるところにてつくられ地の底所にて妙につづりあはされしとき わが骨なんぢにかくるることなかりき
Mifupa yangu haikusitirika kwako nilipoumbwa kwa siri, nilipoumbwa kwa ustadi pande za chini za nchi.
16 わが體いまだ全からざるに なんぢの目ははやくより之をみ 日々かたちづくられしわが百體の一だにあらざりし時に ことごとくなんぢの冊にしるされたり
Uliniona ndani ya tumbo; siku zote zilizo pangwa kwangu ziliandikwa kitabuni mwako hata kabla ya siku ya kwanza kutokea.
17 神よなんぢりもろもろの思念はわれに寶きこといかばかりぞや そのみおもひの総計はいかに多きかな
Ni jinsi gani mawazo yako ni ya thamani kwangu, Mungu! Njinsi ilivyo kubwa jumla zake!
18 我これを算へんとすれどもそのかずは沙よりもおほし われ眼さむるときも尚なんぢとともにをる
Kama nikijaribu kuyahesabu ni mengi kuliko mchanga. Niamkapo bado niko na wewe.
19 神よなんぢはかならず惡者をころし給はん されば血をながすものよ我をはなれされ
Ee Mungu, kama ungewaua waovu; ondokeni kwangu enyi watu wenye vurugu.
20 かれらはあしき企圖をもて汝にさからひて言ふ なんぢの仇はみだりに聖名をとなふるなり
Wanakuasi wewe na kutenda udanganyifu; adui zako wananena uongo.
21 ヱホバよわれは汝をにくむ者をにくむにあらずや なんぢに逆ひておこりたつものを厭ふにあらずや
Je, siwachukii hao, wale wakuchukiao Yahwe? Je, siwadharau wale wanao inuka dhidi yako?
22 われ甚くかれらをにくみてわが仇とす
Nawachukia kabisa; wamekuwa adui zangu.
23 神よねがはくは我をさぐりてわが心をしり 我をこころみてわがもろもろの思念をしりたまへ
Ee Mungu, unichunguze na kuujua moyo wangu; unijaribu na uyajue mawazo yangu.
24 ねがはくは我によこしまなる途のありやなしやを見て われを永遠のみちに導きたまへ
Uone kama kuna njia ya uovu ndani yangu, na uniongoze katika njia ya milele.

< 詩篇 139 >