< 詩篇 112 >

1 主をほめたたえよ。主をおそれて、そのもろもろの戒めを大いに喜ぶ人はさいわいである。
Msifuni Yahwe. Amebarikiwa mtu yule anaye mtii Yahwe, apendezwaye sana na amri zake.
2 その子孫は地において強くなり、正しい者のやからは祝福を得る。
Kizazi chake kitakuwa ni chenye nguvu duniani; kizazi cha mcha Mungu kitabarikiwa.
3 繁栄と富とはその家にあり、その義はとこしえに、うせることはない。
Nyumbani mwake mna utajiri na mali; na haki yake itadumu milele.
4 光は正しい者のために暗黒の中にもあらわれる。主は恵み深く、あわれみに満ち、正しくいらせられる。
Nuru huangazia gizani kwa ajili ya mtu mcha Mungu; yeye ni wa fadhili, huruma, na haki.
5 恵みを施し、貸すことをなし、その事を正しく行う人はさいわいである。
Heri atendaye fadhili na kukopesha, afanyaye mambo yake kwa uaminifu.
6 正しい人は決して動かされることなく、とこしえに覚えられる。
Kwa maana hataondoshwa kamwe; mwenye haki atakumbukwa milele.
7 彼は悪いおとずれを恐れず、その心は主に信頼してゆるがない。
Haogopi habari mbaya; ni jasiri, akimtumainia Yahwe.
8 その心は落ち着いて恐れることなく、ついにそのあだについての願いを見る。
Moyo wake ni mtulivu, hana woga, mpaka aonapo ushindi dhidi ya watesi wake.
9 彼は惜しげなく施し、貧しい者に与えた。その義はとこしえに、うせることはない。その角は誉を得てあげられる。
Huwapa masikini kwa ukarimu; haki yake yadumu milele; atainuliwa kwa heshima.
10 悪しき者はこれを見て怒り、歯をかみならして溶け去る。悪しき者の願いは滅びる。
Mtu mwovu ataona haya na kukasirika; atasaga meno yake na kuyeyuka; tamaa ya wasio haki itapotea.

< 詩篇 112 >