< 詩篇 107 >

1 「主に感謝せよ、主は恵みふかく、そのいつくしみはとこしえに絶えることがない」と、
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 主にあがなわれた者は言え。主は彼らを悩みからあがない、
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 もろもろの国から、東、西、北、南から彼らを集められた。
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 彼らは人なき荒野にさまよい、住むべき町にいたる道を見いださなかった。
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 彼らは飢え、またかわき、その魂は彼らのうちに衰えた。
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから助け出し、
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 住むべき町に行き着くまで、まっすぐな道に導かれた。
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 主はかわいた魂を満ち足らせ、飢えた魂を良き物で満たされるからである。
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 暗黒と深いやみの中にいる者、苦しみと、くろがねに縛られた者、
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 彼らは神の言葉にそむき、いと高き者の勧めを軽んじたので、
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 主は重い労働をもって彼らの心を低くされた。彼らはつまずき倒れても、助ける者がなかった。
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い、
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 暗黒と深いやみから彼らを導き出して、そのかせをこわされた。
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 主は青銅のとびらをこわし、鉄の貫の木を断ち切られたからである。
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 ある者はその罪に汚れた行いによって病み、その不義のゆえに悩んだ。
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 彼らはすべての食物をきらって、死の門に近づいた。
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い、
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 そのみ言葉をつかわして、彼らをいやし、彼らを滅びから助け出された。
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 彼らが感謝のいけにえをささげ、喜びの歌をもって、そのみわざを言いあらわすように。
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 舟で海にくだり、大海で商売をする者は、
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 主のみわざを見、また深い所でそのくすしきみわざを見た。
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 主が命じられると暴風が起って、海の波をあげた。
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 彼らは天にのぼり、淵にくだり、悩みによってその勇気は溶け去り、
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 酔った人のようによろめき、よろめいて途方にくれる。
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 彼らはその悩みのうちに主に呼ばわったので、主は彼らをその悩みから救い出された。
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 主があらしを静められると、海の波は穏やかになった。
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 こうして彼らは波の静まったのを喜び、主は彼らをその望む港へ導かれた。
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 どうか、彼らが主のいつくしみと、人の子らになされたくすしきみわざとのために、主に感謝するように。
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 彼らが民の集会で主をあがめ、長老の会合で主をほめたたえるように。
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 主は川を野に変らせ、泉をかわいた地に変らせ、
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 肥えた地をそれに住む者の悪のゆえに塩地に変らせられる。
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 主は野を池に変らせ、かわいた地を泉に変らせ、
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 飢えた者をそこに住まわせられる。こうして彼らはその住むべき町を建て、
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 畑に種をまき、ぶどう畑を設けて多くの収穫を得た。
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 主が彼らを祝福されたので彼らは大いにふえ、その家畜の減るのをゆるされなかった。
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 彼らがしえたげと、悩みと、悲しみとによって減り、かつ卑しめられたとき、
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 主はもろもろの君に侮りをそそぎ、道なき荒れ地にさまよわせられた。
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 しかし主は貧しい者を悩みのうちからあげて、その家族を羊の群れのようにされた。
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 正しい者はこれを見て喜び、もろもろの不義はその口を閉じた。
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 すべて賢い者はこれらの事に心をよせ、主のいつくしみをさとるようにせよ。
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< 詩篇 107 >