< 箴言 知恵の泉 19 >

1 正しく歩む貧しい者は、曲ったことを言う愚かな者にまさる。
Afadhali mtu maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama, kuliko mpumbavu ambaye midomo yake imepotoka.
2 人が知識のないのは良くない、足で急ぐ者は道に迷う。
Sio vizuri kuwa na juhudi bila maarifa, wala kufanya haraka na kuikosa njia.
3 人は自分の愚かさによって道につまずき、かえって心のうちに主をうらむ。
Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake hata hivyo moyo wake humkasirikia Bwana.
4 富は多くの新しい友を作る、しかし貧しい人はその友に捨てられる。
Mali huleta marafiki wengi, bali rafiki wa mtu maskini humwacha.
5 偽りの証人は罰を免れない、偽りをいう者はのがれることができない。
Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo hataachwa huru.
6 気前のよい人にこびる者は多い、人はみな贈り物をする人の友となる。
Wengi hujipendekeza kwa mtawala na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.
7 貧しい者はその兄弟すらもみなこれを憎む、ましてその友はこれに遠ざからないであろうか。言葉をかけてこれを呼んでも、去って帰らないのである。
Mtu maskini huepukwa na ndugu zake wote: Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani! Ingawa huwafuata kwa kuwasihi, hawapatikani popote.
8 知恵を得る者は自分の魂を愛し、悟りを保つ者は幸を得る。
Yeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe, yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.
9 偽りの証人は罰を免れない、偽りをいう者は滅びる。
Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo ataangamia.
10 愚かな者が、ぜいたくな暮しをするのは、ふさわしいことではない、しもべたる者が、君たる者を治めるなどは、なおさらである。
Haistahili mpumbavu kuishi katika anasa, itakuwa vibaya kiasi gani kwa mtumwa kuwatawala wakuu.
11 悟りは人に怒りを忍ばせる、あやまちをゆるすのは人の誉である。
Hekima ya mtu humpa uvumilivu, ni kwa utukufu wake kusamehe makosa.
12 王の怒りは、ししのほえるようであり、その恵みは草の上におく露のようである。
Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba, bali wema wake ni kama umande juu ya nyasi.
13 愚かな子はその父の災である、妻の争うのは、雨漏りの絶えないのとひとしい。
Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye, naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha.
14 家と富とは先祖からうけつぐもの、賢い妻は主から賜わるものである。
Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Bwana.
15 怠りは人を熟睡させる、なまけ者は飢える。
Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa.
16 戒めを守る者は自分の魂を守る、み言葉を軽んじる者は死ぬ。
Yeye ambaye hutii mafundisho huulinda uhai wake, bali yeye anayezidharau njia zake atakufa.
17 貧しい者をあわれむ者は主に貸すのだ、その施しは主が償われる。
Yeye amhurumiaye maskini humkopesha Bwana, naye atamtuza kwa aliyotenda.
18 望みのあるうちに、自分の子を懲らせ、これを滅ぼす心を起してはならない。
Mrudi mwanao, kwa maana katika hiyo kuna tumaini, usiwe mshirika katika mauti yake.
19 怒ることの激しい者は罰をうける、たとい彼を救ってやっても、さらにくり返さねばならない。
Mtu mwenye kukasirika haraka ni lazima atapata adhabu yake, kama utamwokoa, itakubidi kufanya hivyo tena.
20 勧めを聞き、教訓をうけよ、そうすれば、ついには知恵ある者となる。
Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho, nawe mwishoni utakuwa na hekima.
21 人の心には多くの計画がある、しかしただ主の、み旨だけが堅く立つ。
Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu, lakini kusudi la Bwana ndilo litakalosimama.
22 人に望ましいのは、いつくしみ深いことである、貧しい人は偽りをいう人にまさる。
Lile mtu alionealo shauku ni upendo usio na mwisho, afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.
23 主を恐れることは人を命に至らせ、常に飽き足りて、災にあうことはない。
Kumcha Bwana huongoza kwenye uzima, kisha mtu hupumzika akiwa ameridhika, bila kuguswa na shida.
24 なまけ者は、手を皿に入れても、それを口に持ってゆくことをしない。
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, lakini hawezi hata kuupeleka kwenye kinywa chake!
25 あざける者を打て、そうすれば思慮のない者も慎む。さとき者を戒めよ、そうすれば彼は知識を得る。
Mpige mwenye mzaha, naye mjinga atajifunza busara, mkemee mwenye ufahamu naye atapata maarifa.
26 父に乱暴をはたらき、母を追い出す者は、恥をきたらし、はずかしめをまねく子である。
Yeye amwibiaye baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana aletaye aibu na fedheha.
27 わが子よ、知識の言葉をはなれて人を迷わせる教訓を聞くことをやめよ。
Mwanangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, utatangatanga mbali na maneno ya maarifa.
28 悪い証人はさばきをあざけり、悪しき者の口は悪をむさぼり食う。
Shahidi mla rushwa hudhihaki hukumu na kinywa cha mtu mwovu humeza ubaya kwa upesi.
29 さばきはあざける者のために備えられ、むちは愚かな者の背のために備えられる。
Adhabu zimeandaliwa kwa ajili ya wenye dhihaka na mapigo kwa ajili ya migongo ya wapumbavu.

< 箴言 知恵の泉 19 >