< 箴言 知恵の泉 16 >

1 心にはかることは人に属し、舌の答は主から出る。
Mipango ya moyoni ni ya mwanadamu, bali jibu la ulimi hutoka kwa Bwana.
2 人の道は自分の目にことごとく潔しと見える、しかし主は人の魂をはかられる。
Njia zote za mtu huonekana safi machoni pake mwenyewe, bali makusudi hupimwa na Bwana.
3 あなたのなすべき事を主にゆだねよ、そうすれば、あなたの計るところは必ず成る。
Mkabidhi Bwana lolote ufanyalo, nayo mipango yako itafanikiwa.
4 主はすべての物をおのおのその用のために造り、悪しき人をも災の日のために造られた。
Bwana hufanya kila kitu kwa kusudi lake mwenyewe; hata waovu kwa siku ya maangamizi.
5 すべて心に高ぶる者は主に憎まれる、確かに、彼は罰を免れない。
Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo. Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.
6 いつくしみとまことによって、とがはあがなわれる、主を恐れることによって、人は悪を免れる。
Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa; kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.
7 人の道が主を喜ばせる時、主はその人の敵をもその人と和らがせられる。
Njia za mtu zinapompendeza Bwana, huwafanya hata adui zake waishi naye kwa amani.
8 正義によって得たわずかなものは、不義によって得た多くの宝にまさる。
Afadhali kitu kidogo pamoja na haki kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
9 人は心に自分の道を考え計る、しかし、その歩みを導く者は主である。
Moyo wa mtu huifikiri njia yake, bali Bwana huelekeza hatua zake.
10 王のくちびるには神の決定がある、さばきをするとき、その口に誤りがない。
Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu, wala kinywa chake hakipotoshi haki.
11 正しいはかりと天びんとは主のものである、袋にあるふんどうもすべて彼の造られたものである。
Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana; mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.
12 悪を行うことは王の憎むところである、その位が正義によって堅く立っているからである。
Wafalme huchukia sana kutenda maovu, kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.
13 正しいくちびるは王に喜ばれる、彼は正しい事を言う者を愛する。
Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu; humthamini mtu asemaye kweli.
14 王の怒りは死の使者である、知恵ある人はこれをなだめる。
Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti, bali mtu mwenye hekima ataituliza.
15 王の顔の光には命がある、彼の恵みは春雨をもたらす雲のようだ。
Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai; upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli.
16 知恵を得るのは金を得るのにまさる、悟りを得るのは銀を得るよりも望ましい。
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu, kuchagua ufahamu kuliko fedha!
17 悪を離れることは正しい人の道である、自分の道を守る者はその魂を守る。
Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya; yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake.
18 高ぶりは滅びにさきだち、誇る心は倒れにさきだつ。
Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.
19 へりくだって貧しい人々と共におるのは、高ぶる者と共にいて、獲物を分けるにまさる。
Ni afadhali kuwa mnyenyekevu katika roho miongoni mwa walioonewa kuliko kugawana nyara pamoja na wenye kiburi.
20 慎んで、み言葉をおこなう者は栄える、主に寄り頼む者はさいわいである。
Yeyote anayekubali mafundisho hustawi, tena amebarikiwa yeye anayemtumaini Bwana.
21 心に知恵ある者はさとき者ととなえられる、くちびるが甘ければ、その教に人を説きつける力を増す。
Wenye hekima moyoni huitwa wenye ufahamu, na maneno ya kupendeza huchochea mafundisho.
22 知恵はこれを持つ者に命の泉となる、しかし、愚かさは愚かな者の受ける懲しめである。
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wale walio nao, bali upumbavu huleta adhabu kwa wapumbavu.
23 知恵ある者の心はその言うところを賢くし、またそのくちびるに人を説きつける力を増す。
Moyo wa mtu mwenye hekima huongoza kinywa chake, na midomo yake huchochea mafundisho.
24 ここちよい言葉は蜂蜜のように、魂に甘く、からだを健やかにする。
Maneno ya kupendeza ni kama sega la asali, ni matamu kwa nafsi na uponyaji kwenye mifupa.
25 人が見て自分で正しいとする道があり、その終りはついに死にいたる道となるものがある。
Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu, bali mwisho wake huelekeza mautini.
26 ほねおる者は飲食のためにほねおる、その口が自分に迫るからである。
Shauku ya mfanyakazi humhimiza kufanya kazi; njaa yake humsukuma aendelee.
27 よこしまな人は悪を企てる、そのくちびるには激しい火のようなものがある。
Mtu mbaya kabisa hupanga mabaya, maneno yake ni kama moto uunguzao.
28 偽る者は争いを起し、つげ口する者は親しい友を離れさせる。
Mtu mpotovu huchochea ugomvi, nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.
29 しえたげる者はその隣り人をいざない、これを良くない道に導く。
Mtu mkali humvuta jirani yake na kumwongoza katika mapito yale mabaya.
30 めくばせする者は悪を計り、くちびるを縮める者は悪事をなし遂げる。
Yeye akonyezaye kwa jicho lake anapanga upotovu; naye akazaye midomo yake amenuia mabaya.
31 しらがは栄えの冠である、正しく生きることによってそれが得られる。
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.
32 怒りをおそくする者は勇士にまさり、自分の心を治める者は城を攻め取る者にまさる。
Ni afadhali mtu mstahimilivu kuliko shujaa, mtu anayeitawala hasira yake kuliko yule autekaye mji.
33 人はくじをひく、しかし事を定めるのは全く主のことである。
Kura hupigwa kwa siri, lakini kila uamuzi wake hutoka kwa Bwana.

< 箴言 知恵の泉 16 >