< 箴言 知恵の泉 14 >

1 知恵はその家を建て、愚かさは自分の手でそれをこわす。
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 まっすぐに歩む者は主を恐れる、曲って歩む者は主を侮る。
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 愚かな者の言葉は自分の背にむちを当てる、知恵ある者のくちびるはその身を守る。
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 牛がなければ穀物はない、牛の力によって農作物は多くなる。
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 真実な証人はうそをいわない、偽りの証人はうそをつく。
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 あざける者は知恵を求めても得られない、さとき者は知識を得ることがたやすい。
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 愚かな者の前を離れ去れ、そこには知識の言葉がないからである。
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 さとき者の知恵は自分の道をわきまえることにあり、愚かな者の愚かは、欺くことにある。
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 神は悪しき者をあざけられる、正しい者は、その恵みを受ける。
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 心の苦しみは心みずからが知る、その喜びには他人はあずからない。
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 悪しき者の家は滅ぼされ、正しい者の幕屋は栄える。
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 人が見て自ら正しいとする道でも、その終りはついに死に至る道となるものがある。
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 笑う時にも心に悲しみがあり、喜びのはてに憂いがある。
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 心のもとれる者はそのしわざの実を刈り取り、善良な人もまたその行いの実を刈り取る。
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 思慮のない者はすべてのことを信じる、さとき者は自分の歩みを慎む。
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 知恵ある者は用心ぶかく、悪を離れる、愚かな者は高ぶって用心しない。
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 怒りやすい者は愚かなことを行い、賢い者は忍耐強い。
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 思慮のない者は愚かなことを自分のものとする、さとき者は知識をもって冠とする。
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 悪人は善人の前にひれ伏し、悪しき者は正しい者の門にひれ伏す。
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 貧しい者はその隣にさえも憎まれる、しかし富める者は多くの友をもつ。
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 隣り人を卑しめる者は罪びとである、貧しい人をあわれむ者はさいわいである。
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 悪を計る者はおのれを誤るではないか、善を計る者にはいつくしみと、まこととがある。
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 すべての勤労には利益がある、しかし口先だけの言葉は貧乏をきたらせるだけだ。
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 知恵ある者の冠はその知恵である、愚かな者の花の冠はただ愚かさである。
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 まことの証人は人の命を救う、偽りを吐く者は裏切者である。
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 主を恐れることによって人は安心を得、その子らはのがれ場を得る。
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 主を恐れることは命の泉である、人を死のわなからのがれさせる。
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 王の栄えは民の多いことにあり、君の滅びは民を失うことにある。
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 怒りをおそくする者は大いなる悟りがあり、気の短い者は愚かさをあらわす。
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 穏やかな心は身の命である、しかし興奮は骨を腐らせる。
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 貧しい者をしえたげる者はその造り主を侮る、乏しい者をあわれむ者は、主をうやまう。
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 悪しき者はその悪しき行いによって滅ぼされ、正しい者はその正しきによって、のがれ場を得る。
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 知恵はさとき者の心にとどまり、愚かな者の心に知られない。
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 正義は国を高くし、罪は民をはずかしめる。
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 賢いしもべは王の恵みをうけ、恥をきたらす者はその怒りにあう。
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< 箴言 知恵の泉 14 >