< ヨブ 記 38 >

1 この時、主はつむじ風の中からヨブに答えられた、
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 「無知の言葉をもって、神の計りごとを暗くするこの者はだれか。
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 あなたは腰に帯して、男らしくせよ。わたしはあなたに尋ねる、わたしに答えよ。
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 わたしが地の基をすえた時、どこにいたか。もしあなたが知っているなら言え。
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 あなたがもし知っているなら、だれがその度量を定めたか。だれが測りなわを地の上に張ったか。
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 その土台は何の上に置かれたか。その隅の石はだれがすえたか。
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 かの時には明けの星は相共に歌い、神の子たちはみな喜び呼ばわった。
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 海の水が流れいで、胎内からわき出たとき、だれが戸をもって、これを閉じこめたか。
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 あの時、わたしは雲をもって衣とし、黒雲をもってむつきとし、
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 これがために境を定め、関および戸を設けて、
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 言った、『ここまで来てもよい、越えてはならぬ、おまえの高波はここにとどまるのだ』と。
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 あなたは生れた日からこのかた朝に命じ、夜明けにその所を知らせ、
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 これに地の縁をとらえさせ、悪人をその上から振り落させたことがあるか。
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 地は印せられた土のように変り、衣のようにいろどられる。
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 悪人はその光を奪われ、その高くあげた腕は折られる。
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 あなたは海の源に行ったことがあるか。淵の底を歩いたことがあるか。
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 死の門はあなたのために開かれたか。あなたは暗黒の門を見たことがあるか。
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 あなたは地の広さを見きわめたか。もしこれをことごとく知っているならば言え。
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 光のある所に至る道はいずれか。暗やみのある所はどこか。
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 あなたはこれをその境に導くことができるか。その家路を知っているか。
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 あなたは知っているだろう、あなたはかの時すでに生れており、またあなたの日数も多いのだから。
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 あなたは雪の倉にはいったことがあるか。ひょうの倉を見たことがあるか。
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 これらは悩みの時のため、いくさと戦いの日のため、わたしがたくわえて置いたものだ。
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 光の広がる道はどこか。東風の地に吹き渡る道はどこか。
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 だれが大雨のために水路を切り開き、いかずちの光のために道を開き、
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 人なき地にも、人なき荒野にも雨を降らせ、
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 荒れすたれた地をあき足らせ、これに若草をはえさせるか。
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 雨に父があるか。露の玉はだれが生んだか。
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 氷はだれの胎から出たか。空の霜はだれが生んだか。
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 水は固まって石のようになり、淵のおもては凍る。
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 あなたはプレアデスの鎖を結ぶことができるか。オリオンの綱を解くことができるか。
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 あなたは十二宮をその時にしたがって引き出すことができるか。北斗とその子星を導くことができるか。
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 あなたは天の法則を知っているか、そのおきてを地に施すことができるか。
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 あなたは声を雲にあげ、多くの水にあなたをおおわせることができるか。
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 あなたはいなずまをつかわして行かせ、『われわれはここにいる』と、あなたに言わせることができるか。
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 雲に知恵を置き、霧に悟りを与えたのはだれか。
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 だれが知恵をもって雲を数えることができるか。だれが天の皮袋を傾けて、
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 ちりを一つに流れ合させ、土くれを固まらせることができるか。
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 あなたはししのために食物を狩り、子じしの食欲を満たすことができるか。
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 彼らがほら穴に伏し、林のなかに待ち伏せする時、あなたはこの事をなすことができるか。
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 からすの子が神に向かって呼ばわり、食物がなくて、さまようとき、からすにえさを与える者はだれか。
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< ヨブ 記 38 >