< Uromawa 9 >

1 Ma buka shi kadundure anyimo ani za ni kiristi, inda boom macico ba, iriba im ibezizim imum ibibe biriri.
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 Ami, inzin ina puru abit wan unu pazaza iriba izatu umarsa
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Barki mi, unyara um acari mini sarki. Yesu nan anu henu um an desa wazi am, anyimo amagasiya mani pum.
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 Wee wani A'israila wa hem unu rii nan innu u'inko utize wan unu nyanki ubara utize nan ninonzo ni ugomo Asere kasi inda sa ma ziki.
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 Ani lem niwe nini Yesu ma suri nin, ugomo Asere maa wu we ni lem ni riri. I cukuno ani me. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Barki ani me ida zoo gu tize ti ugomo Asere ta rizo ba. Daki vat desa ma raa a usraila ma cukuno u'israila ba.
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 Ane ani daki vat bisana bi Ibrahim wa cukuno ahana ame ba. Usuro u Ishaka adi ku guna bisana bi shi me ba tubusa ni.
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 Ane ani ahanaa ani pum wa d a zo we ahanaa Asere ba. Ahanaa ubarka utize we wa cukuno bisana bi meme.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 Ane ani ubarka utize me wa cukuno. Uganiya ugeme indi e in nya Saraya vanaa uruma
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 Daki ane ani cas ba Saratu ma wuu apuru nan ure unu sa ma cukuno acoo aru me mani Ishaku.
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 Daki amu yoo ahana me ba nani agu wamu wuza imum iriri nani izenze, bati unyara ugomo Asere udi cukuno abizauka, daki ahira akatu ma ba, idi cukuno ahira adesa ma tita duru.
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 Agun me unanu me madi wuzi unu uneze umeme ni rere.
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 Ane ani anyerttike, “ma hem in Yakubu ma nyaru in Isuwa”.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Haru tiku gu nyani ni? Ure usizikime ahira Ugomo Asere urani, ka iwu ani me ba haa.
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Ma gun in Musa “indi kunna desa indi kunna me, indi ori desa in kunna urunta ume.”
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 Ane ani, daki barki unyara ume ba, nani usum ume ba, barki Ugomo Asere desa mabezi usheu.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Tize ti Ugomo Asere ta gun in Fir'auna, barki imum igeme ma yeze we bati in bezi nikara ahira awe me, bati niza num nikuri, ni ribe anyimo une vat.
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 Ane ani Ugomo Asere ma kunna ugogoni udebe sa ma zauka, uye wu me ma cukuno gbas.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Idi iki ni mi igu, “nyanini ya wuna ugomo Asere ma nyara ukem usiziki anice na nu?”, aveni ma dake ma ri nikara ni ruba imeme?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 A ure uhira, hu aveni sa wa bari uvovi bigiri nan Ugomo Asere? Adake akem imum sa uye ma bara i gun desa ma bara ini “nyanini ya wuna wa barkam ani me?”
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Nani unu bara umuharu muti nyanga mada zoo me in nikara inguna ma wuzi katuma ku ira iriba imeme ba. Mada ke ma barka imum iriri nan izenze.
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 Nyanini idi cukuno, inki me ugomo desa ma nyara ma bezi ucornome iriba imeme ma bezi ubari umeme amasaa.
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 Anyimo ani me make ma natti iriba kang ahira ubezi ucorno me iriba sa i bee uhuza anu ahuma? nyanini idi cukuno, inki ma wuza imum igeme bati ma bezi ninonzo ni meme anice ni iriba ineze imeme ahira ani nonzo ni meme.
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 Nyanini, inki ma wuza imum igeme barki haru, de sa ma titin duru haru sa tida zo me Ayahudawa, haru andesa wazi ana madini.
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 Kasi inda be sa ma buka anyimo unyertike uHosiya unu guna “An de sa wa zowe am wa cukuno am, anu me sa ma gam we in gu ma hem in we”.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 Rep, ahira me sa aguna wa zoo we am, abini me adi gun we ahana Asere.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 Ishaya maa poki anyo abanga anu U'israila ma gu, “inki anu u'israila wa cukuno gbardang kasi bikiki bi uraba udang, ukasu uni adi buri we”.
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 Sarki udondonkino Ugmo Asere madi wuzi katuma ka meme anyimo unee vat ma mari.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 Ishaya ma kuri ma buki “sarki Ugomo Asere unu bari ma ceki bisana adumo barki haru ba, tida cukuno gusi Usodom tida zina kasi Ugomora.''
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Tiduku guna nyanini? ana madini me sa daki lau ba, waye wa sana, ukem ulau barki uhem wasere.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 A Israilawa sa wa wuzi morso mu nyara tarsa una uriri wasere, daki wa kem ba.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Nyanini ya ayen ani me? barki daki wa nyari ini iriba i inde ba, yaa cukuno ahira atuma kani. we wonno wa pilliko ani poo nu wuza upillizino.
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 kasi unyertike utize tu ugomo Asere ta buka “mi be ma nukka nipoo Usihiyona, nipoo nupilko sa nidi wuu anu wa rizi. Vat desa ma hem mada kunna me mu'ii ba.''
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Uromawa 9 >