< Uluka 13 >

1 Uganiya, ara anu wa buki me Bilatus wa are galilawa samapatti maye ma weme nan nu hadaya uweme.
Kwa wakataihuo huo, kulikuwa na baadhi watu waliomtaarifu juu ya Wagalilaya ambao Pilato aliwaua na kuchanganya damu yao na sadaka zao.
2 Yeso mabirka we, Ibassa a Galilawa wagino wateki ukasu me in madini, sa wa ziti anime?
Yesu akajibu na kuwaambia, “Je mwadhani kuwa Wagalilaya hao walikuwa na dhambi kuliko Wagalilaya wengine wote ndiyo maana wamepatwa na mabaya hayo?
3 A, a in bo shi, inda ya nya a acce ashime, lali wii kasi weme.
Hapana, nawaambia, lakini msipotubu, nanyi mtaangamia vivyo hivyo.
4 Nyani gusi anu siluwam ukirau ina nu witi-tari gino u husmiya wa rizi a we uhuu we, ibassa wateki ukasu wanu Urushalima vat unu cara abanga?
Au wale watu kumi na nane katika Siloamu ambao mnara ulianguka na kuwaua, mnafikiri wao walikuwa wenye dhambi zaidi kuliko watu wengine katika Yerusalemu?
5 Inpo shi izome ani mani, vat de sa daki manya nicce vat uwe wadi wii,
Hapana, mimi nasema, lakini kama msipotubu, ninyi nyote pia mtaangamia.
6 Yeso mabuki agino me, ure unu ma biri upom urung inabi umeme unyara a hana dakimā kem ba.
Yesu aliwaambia mfano huu, “Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake na alikwenda kutafuta matunda juu yake lakini hakupata.
7 Madusa magu inde sa ma hira urung me, tiiue ta zige me in ezizze ahing upom ugeme agi ingazi in iremum mun ba. Ca akorko uni, A wuzi aneni a ceki uni ukursu ahira me hem anime?
Akamwambia mtunza bustani, 'Tazama, kwa miaka mitatu nimekuja na kujaribu kutafuta matunda kwenye mtini huu lakini sikupata. Uukate. Kwani ulete uharibifu wa ardhi?
8 Deusa mahira urung me magu, nya uni uganiya cingun in butuko in wuu uni utenki.
Mtunza bustani akajibu na kusema, 'uache mwaka huu ili niupalilie na kuweka mbolea juu yake.
9 Inki wa yoo ani wee nu kuro, a memerum ini nome.
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, ni vema; lakini kama hautazaa, uukate!”'
10 Ure uwui Yeso mazinu bezi utize, Bono me Asabar ani azi.
Sasa Yesu alikuwa akifundisha katika mojawapo ya Masinagogi wakati wa Sabato.
11 Ure uce mawu tiwe ukirau intini witi-tari mazin unu koni uzenze, ma ciki tungoron, da ma rusi utonno ba.
Tazama, alikuwepo mama mmoja ambaye kwa miaka kumi na minane alikuwa na rohomchafu wa udhaifu, na yeye alikuwa amepinda na hana uwezo kabisa wa kusimama.
12 Yeso ma iri me, ma ti ti me magun me, ukoni ugame ma humawe uni,
Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umewekwa huru kutoka kwenye udhaifu wako.”
13 Yeso ma tāri-tāri a me, ma dusa mahiri matonno madusa nonzo Asere.
Akaweka mikono yake juu yake, na mara mwili wake akajinyoosha na akamtukuza Mungu.
14 Abanna me, una je udenge utize ta sere ma guna iruba barki Yeso mahuma unu rono Asabaci. Unaje magu ma anu, “Tu wui utasi tirani sa unu madake mawuzi katuma. Ayeni a humza shi, kati I ezi rono Asabaci ba.
Lakini mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo mtawala akajibu akawambia makutano, “Kuna siku sita ambazo ni lazima kufanya kazi. Njoni kuponywa basi, si katika siku ya Sabato. '
15 Abinime Ugomo-Asere, makabirka me, Ana Iriba ibit! Ida sapso shi izenki ishi me nyani inna amatu-kum maweme ika nyani we gmei rono Asabaci?
Bwana akamjibu na akasema, “wanafiki! Hakuna kila mmoja wenu kufungua punda wako au ng'ombe kutoka zizini na kuwaongoza kumpeleka kunywa siku ya Sabato?
16 Uca wa kura Ibrahim, de sa bibe bi buru ba tirza tiwe ukirau in tini witi-tari. Adake a sapi me rono asabaci ba?
Hivyo pia binti wa Abrahamu, ambaye Shetani amemfunga kwa miaka kumi na minane, je haikumpasa kifungo chake kisifunguliwe siku ya sabato?”
17 Sa buka anime vat ande sa nyare me wa kunna mu eh, vat ana ori wa wu iriba irom in ti mum ti humma sa mawuzi.
Alipokuwa akisema maneno hayo, wale wote waliompinga waliona aibu, bali makutano wote wa wengine walishangilia kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyotenda.
18 Yeso maguana, “Ane ni adi iri tigomo ta Sere, indi kuri inki tini aneni?
Yesu akasema, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini, na naweza kuulinganisha na nini?
19 Izi kasi biho bi ukungu, sa ure unu mabiri anyimo urung umeme, usuri uzi uwuu bi titi bi dandang, inyi Ibara tisu iriri me.
Ni kama mbegu ya haradari aliyoitwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake, na ikamea ikawa mti mkubwa, na ndege wa mbinguni wakajenga viota vyao katika matawi yake.
20 Makuri magu, in Nyanini indi bati in tigomo ta Sere?
Tena akasema, “Niufananishe na nini ufalme wa Mungu?
21 Tizi kasi uyist sa ure uneh ma pitti nan mudu mataru mumu ina ma alkama bati mupoo.
Ni kama chachu ambayo mwanamke aliichukua na kuchanganyakwenye vipimo vitatu vya unga hata ukaumuka.”
22 Yeso māha ati pin nan na giro, una me sa hazi Urushalima mabezi we tize ta Sere.
Yesu alitembelea kila mji na kijiji njiani akielekea Yerusalemu na kuwafundisha.
23 Uye magun me, “Ugomo-Asere, ande sa adi kabiwe wadizi cingilin ini?” Magunwa,
Mtu mmoja akauliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?” Hivyo akawaambia,
24 Inkoni Iruba iribe ana tukum a shut, barki magunan shi, anu gbardang wadi nyari uribe abanna me wada keme uribe ba.
“Jitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba, kwa sababu wengi watajaribu na hawataweza kuingia.
25 Inki una kura mā impo ana tukum, idi tonno amatara imeki ukpotiko ana tukum me, Ugomo-Asere, tonno tiribe. Madi kabirka magun shi, mi intam shi nan na hira mesa ya suroni.
Mara baada ya mmiliki wa nyumba kusimama na kufunga mlango, basi mtasimama nje na kupiga hodi mlangoni na kusema, Bwana, Bwana, tufungulie yeye atajibu na kuwaambia, siwajui ninyi wala mtokako.'
26 Abini me idi gu, 'Tare ta saa a mu henu muweme, wa kuri wa bezizi a tina tiru.
Ndipo mtasema, Tulikula na kunywa mbele yako na wewe ulifundisha katika mitaa yetu.”
27 Abanna me madi kabirka, magu, “In boshi, intam nyani abani ya suroni ba. Seserken mi upuro, vat ushi anu wuza imum izenze!
Lakini yeye atawajibu, `nawaambia, siwajui mtokako, ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!'
28 Adi shii a romsi ahiini uganiya sa ya ira Ibrahim, nan Ishaku nan Yakubu wanu vat ana kadura ka sere a tigomo ta Asere.
Kutakuwa na kilio na kusaga meno wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mumetupwa nje.
29 Wadi ezi usoro ugabas, uwatu dizii, ukudu nan Arewa, wadi re utebiri umari utigomo ta Sere.
Watafika kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, na kupumzika katika meza ya chakula cha jioni katika ufalme wa Mungu.
30 Irusi ini gino me, ana dumo wadi cukuno anaje, ana je wakuri wa cukuno ana dumo.”
Na tambua hili, wa mwisho ni wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho.”
31 Ahira-ahirame, are Farisiwa e wa wagun me, “Hira abame Hirudus manyara uhuna uwe.
Muda mfupi baadaye, baadhi ya Mafarisayo walikuja na kumwambia, “Nenda na ondoka hapa kwa sababu Herode anataka kukuua.”
32 Yeso magu, hana ni ika buka udila ugino ugino unuguna, ira, ma suzo a gbergene, in humza inanu koya uwui, uwui ukutaru uni in mari kadumakam.
Yesu akasema, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, `Tazama, ninawafukuza pepo na kufanya uponyaji leo na kesho, na siku ya tatu nitatimiza lengo langu.
33 Indi tarzi vat tina, ya cukuno gbas ini reje in tanu tum kani me nan ni sizo nan urono, barki daki ya wuna ure ahun una kadura ka Sere piit na nu Urushalima ba.
Katika hali yoyote, ni muhimu kwa ajili yangu kuendelea leo, kesho, na siku iliyofuata, kwa vile haikubaliki kumuua nabii mbali na Yerusalemu.
34 Urushalima, Urushalima anu uhuza ana kadura kasere, anu tisa ande sa tumawa ahira aweme. Kani ka hono kani in nyara uguna in ori ahana aweme gusi bitukoro sa bidi ke bi ori ahana abiru anyimo magaure mabini, abanna me unyara anime ba.
Yerusalemu, Yerusalemu, nani anawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu. Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wenu kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini humkulitaka hili.
35 Ira, a humuko a kura aweme. In bo shi sisi, ida kuri irin me ba rono be sa ya guna, imumu ire-re icukuno ahira unu be sa ma eze anyimo aniza nu ugomo-Asere.
Tazama, nyumba yako imetelekezwa. Nami nawaambia, hamuwezi kuniona hata mtakaposema 'Amebarikiwa huyo ajaye kwa jina la Bwana.'”

< Uluka 13 >