< Salmi 78 >

1 Cantico di Asaf. Ascolta, popolo mio, il mio insegnamento; porgete gli orecchi alle parole della mia bocca!
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Io aprirò la mia bocca per proferir parabole, esporrò i misteri de’ tempi antichi.
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Quel che noi abbiamo udito e conosciuto, e che i nostri padri ci hanno raccontato,
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 non lo celeremo ai loro figliuoli; diremo alla generazione avvenire le lodi dell’Eterno, e la sua potenza e le maraviglie ch’egli ha operato.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Egli stabilì una testimonianza in Giacobbe, e pose una legge in Israele, ch’egli ordinò ai nostri padri di far conoscere ai loro figliuoli,
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 perché fossero note alla generazione avvenire, ai figliuoli che nascerebbero, i quali alla loro volta le narrerebbero ai loro figliuoli,
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 ond’essi ponessero in Dio la loro speranza e non dimenticassero le opere di Dio, ma osservassero i suoi comandamenti;
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 e non fossero come i loro padri, una generazione caparbia e ribelle, una generazione dal cuore incostante, e il cui spirito non fu fedele a Dio.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 I figliuoli di Efraim, gente di guerra, buoni arcieri, voltaron le spalle il dì della battaglia.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Non osservarono il patto di Dio, e ricusarono di camminar secondo la sua legge;
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 e dimenticarono le sue opere e i prodigi ch’egli avea loro fatto vedere.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Egli avea compiuto maraviglie in presenza de’ loro padri, nel paese d’Egitto, nelle campagne di Zoan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Fendé il mare e li fece passare, e fermò le acque come in un mucchio.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 Di giorno li guidò con una nuvola, e tutta la notte con una luce di fuoco.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Schiantò rupi nel deserto, e li abbeverò copiosamente, come da gorghi.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Fece scaturire ruscelli dalla roccia e ne fece scender dell’acque a guisa di fiumi.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Ma essi continuarono a peccare contro di lui, a ribellarsi contro l’Altissimo, nel deserto;
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 e tentarono Dio in cuor loro, chiedendo cibo a lor voglia.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 E parlarono contro Dio, dicendo: Potrebbe Dio imbandirci una mensa nel deserto?
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Ecco, egli percosse la roccia e ne colarono acque, ne traboccaron torrenti; potrebb’egli darci anche del pane, e provveder di carne il suo popolo?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Perciò l’Eterno, avendoli uditi, s’adirò fieramente, e un fuoco s’accese contro Giacobbe, e l’ira sua si levò contro Israele,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 perché non aveano creduto in Dio, né avevano avuto fiducia nella sua salvazione;
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 eppure egli comandò alle nuvole di sopra, e aprì le porte del cielo,
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 e fece piover su loro manna da mangiare, e dette loro del frumento del cielo.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 L’uomo mangiò del pane dei potenti; egli mandò loro del cibo a sazietà.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Fece levare in cielo il vento orientale, e con la sua potenza addusse il vento di mezzodì;
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 fece piover su loro della carne come polvere, degli uccelli alati, numerosi come la rena del mare;
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 e li fece cadere in mezzo al loro campo, d’intorno alle loro tende.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 Così essi mangiarono e furon ben satollati, e Dio mandò loro quel che aveano bramato.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Non si erano ancora distolti dalle loro brame, avevano ancora il loro cibo in bocca,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 quando l’ira di Dio si levò contro loro, e ne uccise tra i più fiorenti, e abbatté i giovani d’Israele.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Con tutto ciò peccarono ancora, e non credettero alle sue maraviglie.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 Ond’egli consumò i loro giorni in vanità, e i loro anni in ispaventi.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Quand’ei li uccideva, essi lo ricercavano e tornavano bramosi di ritrovare Iddio;
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 e si ricordavano che Dio era la loro ròcca, l’Iddio altissimo il loro redentore.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Essi però lo lusingavano con la loro bocca, e gli mentivano con la loro lingua.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 Il loro cuore non era diritto verso lui, e non eran fedeli al suo patto.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Ma egli, che è pietoso, che perdona l’iniquità e non distrugge il peccatore, più volte rattenne la sua ira, e non lasciò divampare tutto il suo cruccio.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Ei si ricordò ch’essi erano carne, un fiato che passa e non ritorna.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Quante volte si ribellarono a lui nel deserto, e lo contristarono nella solitudine!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 E tornarono a tentare Iddio e a provocare il Santo d’Israele.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Non si ricordaron più della sua mano, del giorno in cui egli li liberò dal nemico,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 quando operò i suoi miracoli in Egitto, e i suoi prodigi nelle campagne di Zoan;
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 mutò i loro fiumi in sangue, e i loro rivi in guisa che non potean più bere;
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 mandò contro loro mosche velenose che li divoravano, e rane che li distruggevano;
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 dette il loro raccolto ai bruchi e la loro fatica alle locuste;
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 distrusse le loro vigne con la gragnuola e i loro sicomori coi grossi chicchi d’essa;
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 abbandonò il loro bestiame alla grandine e le lor gregge ai fulmini.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Scatenò su loro l’ardore del suo cruccio, ira, indignazione e distretta, una torma di messaggeri di malanni.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Dette libero corso alla sua ira; non preservò dalla morte la loro anima, ma abbandonò la loro vita alla pestilenza.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Percosse tutti i primogeniti d’Egitto, le primizie del vigore nelle tende di Cham;
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 ma fece partire il suo popolo a guisa di pecore, e lo condusse a traverso il deserto come una mandra.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Lo guidò sicuramente sì che non ebbero da spaventarsi, mentre il mare inghiottiva i loro nemici.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 Li fece arrivare alla sua santa frontiera, alla montagna che la sua destra avea conquistato.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Scacciò le nazioni dinanzi a loro, ne assegnò loro a sorte il paese quale eredità, e nelle tende d’esse fece abitare le tribù d’Israele.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 E nondimeno tentarono l’Iddio altissimo e si ribellarono e non osservarono le sue testimonianze.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Si trassero indietro e furono sleali come i loro padri; si rivoltarono come un arco fallace;
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 lo provocarono ad ira coi loro alti luoghi, lo mossero a gelosia con le loro sculture.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Dio udì questo, e si adirò, prese Israele in grande avversione,
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 onde abbandonò il tabernacolo di Silo, la tenda ov’era dimorato fra gli uomini;
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 e lasciò menare la sua Forza in cattività, e lasciò cader la sua Gloria in man del nemico.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 Abbandonò il suo popolo alla spada, e s’adirò contro la sua eredità.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Il fuoco consumo i loro giovani, e le loro vergini non ebber canto nuziale.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 I loro sacerdoti caddero per la spada, e le loro vedove non fecer lamento.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Poi il Signore si risvegliò come uno che dormisse, come un prode che grida eccitato dal vino.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 E percosse i suoi nemici alle spalle, e mise loro addosso un eterno vituperio.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 Ma ripudiò la tenda di Giuseppe, e non elesse la tribù di Efraim;
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 ma elesse la tribù di Giuda, il monte di Sion ch’egli amava.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 Edificò il suo santuario a guisa de’ luoghi eccelsi, come la terra ch’egli ha fondata per sempre.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 Elesse Davide, suo servitore, lo prese dagli ovili;
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 lo trasse di dietro alle pecore lattanti, per pascere Giacobbe suo popolo, ed Israele sua eredità.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 Ed egli li pasturò secondo l’integrità del suo cuore, e li guidò con mano assennata.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

< Salmi 78 >