< Salmi 78 >

1 Cantico di Asaf. Ascolta, popolo mio, il mio insegnamento; porgete gli orecchi alle parole della mia bocca!
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Io aprirò la mia bocca per proferir parabole, esporrò i misteri de’ tempi antichi.
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Quel che noi abbiamo udito e conosciuto, e che i nostri padri ci hanno raccontato,
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 non lo celeremo ai loro figliuoli; diremo alla generazione avvenire le lodi dell’Eterno, e la sua potenza e le maraviglie ch’egli ha operato.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Egli stabilì una testimonianza in Giacobbe, e pose una legge in Israele, ch’egli ordinò ai nostri padri di far conoscere ai loro figliuoli,
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 perché fossero note alla generazione avvenire, ai figliuoli che nascerebbero, i quali alla loro volta le narrerebbero ai loro figliuoli,
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 ond’essi ponessero in Dio la loro speranza e non dimenticassero le opere di Dio, ma osservassero i suoi comandamenti;
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 e non fossero come i loro padri, una generazione caparbia e ribelle, una generazione dal cuore incostante, e il cui spirito non fu fedele a Dio.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 I figliuoli di Efraim, gente di guerra, buoni arcieri, voltaron le spalle il dì della battaglia.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Non osservarono il patto di Dio, e ricusarono di camminar secondo la sua legge;
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 e dimenticarono le sue opere e i prodigi ch’egli avea loro fatto vedere.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Egli avea compiuto maraviglie in presenza de’ loro padri, nel paese d’Egitto, nelle campagne di Zoan.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Fendé il mare e li fece passare, e fermò le acque come in un mucchio.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 Di giorno li guidò con una nuvola, e tutta la notte con una luce di fuoco.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Schiantò rupi nel deserto, e li abbeverò copiosamente, come da gorghi.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 Fece scaturire ruscelli dalla roccia e ne fece scender dell’acque a guisa di fiumi.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Ma essi continuarono a peccare contro di lui, a ribellarsi contro l’Altissimo, nel deserto;
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 e tentarono Dio in cuor loro, chiedendo cibo a lor voglia.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 E parlarono contro Dio, dicendo: Potrebbe Dio imbandirci una mensa nel deserto?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Ecco, egli percosse la roccia e ne colarono acque, ne traboccaron torrenti; potrebb’egli darci anche del pane, e provveder di carne il suo popolo?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Perciò l’Eterno, avendoli uditi, s’adirò fieramente, e un fuoco s’accese contro Giacobbe, e l’ira sua si levò contro Israele,
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 perché non aveano creduto in Dio, né avevano avuto fiducia nella sua salvazione;
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 eppure egli comandò alle nuvole di sopra, e aprì le porte del cielo,
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 e fece piover su loro manna da mangiare, e dette loro del frumento del cielo.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 L’uomo mangiò del pane dei potenti; egli mandò loro del cibo a sazietà.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Fece levare in cielo il vento orientale, e con la sua potenza addusse il vento di mezzodì;
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 fece piover su loro della carne come polvere, degli uccelli alati, numerosi come la rena del mare;
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 e li fece cadere in mezzo al loro campo, d’intorno alle loro tende.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Così essi mangiarono e furon ben satollati, e Dio mandò loro quel che aveano bramato.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Non si erano ancora distolti dalle loro brame, avevano ancora il loro cibo in bocca,
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 quando l’ira di Dio si levò contro loro, e ne uccise tra i più fiorenti, e abbatté i giovani d’Israele.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Con tutto ciò peccarono ancora, e non credettero alle sue maraviglie.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Ond’egli consumò i loro giorni in vanità, e i loro anni in ispaventi.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Quand’ei li uccideva, essi lo ricercavano e tornavano bramosi di ritrovare Iddio;
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 e si ricordavano che Dio era la loro ròcca, l’Iddio altissimo il loro redentore.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Essi però lo lusingavano con la loro bocca, e gli mentivano con la loro lingua.
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 Il loro cuore non era diritto verso lui, e non eran fedeli al suo patto.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Ma egli, che è pietoso, che perdona l’iniquità e non distrugge il peccatore, più volte rattenne la sua ira, e non lasciò divampare tutto il suo cruccio.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Ei si ricordò ch’essi erano carne, un fiato che passa e non ritorna.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Quante volte si ribellarono a lui nel deserto, e lo contristarono nella solitudine!
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 E tornarono a tentare Iddio e a provocare il Santo d’Israele.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Non si ricordaron più della sua mano, del giorno in cui egli li liberò dal nemico,
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 quando operò i suoi miracoli in Egitto, e i suoi prodigi nelle campagne di Zoan;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 mutò i loro fiumi in sangue, e i loro rivi in guisa che non potean più bere;
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 mandò contro loro mosche velenose che li divoravano, e rane che li distruggevano;
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 dette il loro raccolto ai bruchi e la loro fatica alle locuste;
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 distrusse le loro vigne con la gragnuola e i loro sicomori coi grossi chicchi d’essa;
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 abbandonò il loro bestiame alla grandine e le lor gregge ai fulmini.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 Scatenò su loro l’ardore del suo cruccio, ira, indignazione e distretta, una torma di messaggeri di malanni.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 Dette libero corso alla sua ira; non preservò dalla morte la loro anima, ma abbandonò la loro vita alla pestilenza.
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 Percosse tutti i primogeniti d’Egitto, le primizie del vigore nelle tende di Cham;
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 ma fece partire il suo popolo a guisa di pecore, e lo condusse a traverso il deserto come una mandra.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Lo guidò sicuramente sì che non ebbero da spaventarsi, mentre il mare inghiottiva i loro nemici.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Li fece arrivare alla sua santa frontiera, alla montagna che la sua destra avea conquistato.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 Scacciò le nazioni dinanzi a loro, ne assegnò loro a sorte il paese quale eredità, e nelle tende d’esse fece abitare le tribù d’Israele.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 E nondimeno tentarono l’Iddio altissimo e si ribellarono e non osservarono le sue testimonianze.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 Si trassero indietro e furono sleali come i loro padri; si rivoltarono come un arco fallace;
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 lo provocarono ad ira coi loro alti luoghi, lo mossero a gelosia con le loro sculture.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Dio udì questo, e si adirò, prese Israele in grande avversione,
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 onde abbandonò il tabernacolo di Silo, la tenda ov’era dimorato fra gli uomini;
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 e lasciò menare la sua Forza in cattività, e lasciò cader la sua Gloria in man del nemico.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 Abbandonò il suo popolo alla spada, e s’adirò contro la sua eredità.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Il fuoco consumo i loro giovani, e le loro vergini non ebber canto nuziale.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 I loro sacerdoti caddero per la spada, e le loro vedove non fecer lamento.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Poi il Signore si risvegliò come uno che dormisse, come un prode che grida eccitato dal vino.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 E percosse i suoi nemici alle spalle, e mise loro addosso un eterno vituperio.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Ma ripudiò la tenda di Giuseppe, e non elesse la tribù di Efraim;
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 ma elesse la tribù di Giuda, il monte di Sion ch’egli amava.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Edificò il suo santuario a guisa de’ luoghi eccelsi, come la terra ch’egli ha fondata per sempre.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Elesse Davide, suo servitore, lo prese dagli ovili;
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 lo trasse di dietro alle pecore lattanti, per pascere Giacobbe suo popolo, ed Israele sua eredità.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Ed egli li pasturò secondo l’integrità del suo cuore, e li guidò con mano assennata.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

< Salmi 78 >