< Salmi 56 >

1 Per il Capo de’ musici. Su: “Colomba de’ terebinti lontani”. Inno di Davide quando i Filistei lo presero in Gat. Abbi pietà di me, o Dio, poiché gli uomini anelano a divorarmi; mi tormentano con una guerra di tutti i giorni;
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
2 i miei nemici anelano del continuo a divorarmi, poiché sono molti quelli che m’assalgono con superbia.
Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
3 Nel giorno in cui temerò, io confiderò in te.
Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
4 Coll’aiuto di Dio celebrerò la sua parola; in Dio confido, e non temerò; che mi può fare il mortale?
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
5 Torcon del continuo le mie parole; tutti i lor pensieri son vòlti a farmi del male.
Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
6 Si radunano, stanno in agguato, spiano i miei passi, come gente che vuole la mia vita.
Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
7 Rendi loro secondo la loro iniquità! O Dio, abbatti i popoli nella tua ira!
Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
8 Tu conti i passi della mia vita errante; raccogli le mie lacrime negli otri tuoi; non sono esse nel tuo registro?
Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
9 Nel giorno ch’io griderò, i miei nemici indietreggeranno. Questo io so: che Dio è per me.
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10 Coll’aiuto di Dio celebrerò la sua parola; coll’aiuto dell’Eterno celebrerò la sua parola.
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11 In Dio confido e non temerò; che mi può far l’uomo?
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
12 Tengo presenti i voti che t’ho fatti, o Dio; io t’offrirò sacrifizi di lode;
Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
13 poiché tu hai riscosso l’anima mia dalla morte, hai guardato i miei piedi da caduta, ond’io cammini, al cospetto di Dio, nella luce de’ viventi.
Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.

< Salmi 56 >