< Salmi 73 >

1 Salmo di Asaf CERTAMENTE Iddio [è] buono ad Israele, A [quelli che son] puri di cuore.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Ora, quant'è a me, quasi che incapparono i miei piedi; Come nulla [mancò] che i miei passi non isdrucciolassero.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Perciocchè io portava invidia agl'insensati, Veggendo la prosperità degli empi.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Perciocchè non [vi sono] alcuni legami alla lor morte; E la lor forza [è] prosperosa.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 [Quando] gli [altri] uomini [sono] in travagli, essi non [vi son] punto; E non ricevono battiture col rimanente degli uomini.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Perciò, la superbia li cinge a giusa di collana; La violenza li involge [come] un vestimento.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Gli occhi escono loro fuori per lo grasso; Avanzano le immaginazioni del cuor [loro].
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Son dissoluti, e per malizia ragionano di oppressare; Parlano da alto.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Mettono la lor bocca dentro al cielo, E la lor lingua passeggia per la terra.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Perciò, il popolo di Dio riviene a questo, [Veggendo che] l'acqua gli è spremuta a bere a pien [calice],
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 E dice: Come [può essere che] Iddio sappia [ogni cosa], E che vi sia conoscimento nell'Altissimo?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 Ecco, costoro [son] empi, e pur godono pace e tranquillità in perpetuo; Ed accrescono le [lor] facoltà.
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Indarno [adunque] in vero ho nettato il mio cuore, Ed ho lavate le mie mani nell'innocenza.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 Poichè son battuto tuttodì, Ed ogni mattina il mio gastigamento [si rinnuova].
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Se io dico: Io ragionerò così; Ecco, io son disleale inverso la generazione de' tuoi figliuoli.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Io ho adunque pensato di [volere] intender questo; Ma [la cosa] mi è parsa molto molesta.
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Infino a tanto che sono entrato ne' santuari di Dio; [Ed] ho considerato il fine di coloro.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Certo, tu li metti in isdruccioli; Tu li trabocchi in ruine.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 Come sono eglino stati distrutti in un momento! [Come] son venuti meno, e sono stati consumati per casi spaventevoli!
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 [Son] come un sogno, dopo che [l'uomo] si è destato; O Signore, quando tu [ti] risveglierai, tu sprezzerai la lor vana apparenza.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Quando il mio cuore era inacerbito, Ed io era punto nelle reni;
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 Io [era] insensato, e non aveva conoscimento; Io era inverso te [simile] alle bestie.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Ma pure io sono stato del continuo teco; Tu mi hai preso per la man destra.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Tu mi condurrai per lo tuo consiglio, E poi mi riceverai [in] gloria;
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 Chi [è] per me in cielo, [fuor che te?] Io non voglio [altri] che te in terra.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 La mia carne ed il mio cuore erano venuti meno: [Ma] Iddio [è] la rocca del mio cuore, e la mia parte in eterno.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Perciocchè, ecco, quelli che si allontanano da te periranno; Tu distruggerai ogni uomo che fornica[ndo si svia] da te.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Ma quant'è a me, egli mi [è] buono di accostarmi a Dio; Io ho posta nel Signore Iddio la mia confidanza, Per raccontar tutte le opere sue.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Salmi 73 >