< Salmi 135 >

1 ALLELUIA. Lodate il Nome del Signore; Lodate[lo, voi] servitori del Signore;
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Che state nella Casa del Signore, Ne' cortili della Casa del nostro Dio.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Lodate il Signore; perciocchè il Signore [è] buono; Salmeggiate al suo Nome, perciocchè [è] amabile.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Conciossiachè il Signore si abbia eletto Giacobbe [Ed] Israele per suo tesoro riposto.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Certo io conosco che il Signore [è] grande, E che il nostro Signore [è maggiore] di tutti gl'iddii.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Il Signore fa tutto ciò che gli piace In cielo ed in terra; Ne' mari, ed [in] tutti gli abissi.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Egli fa salire i vapori dall'estremità dalle terra; Egli fa i lampi per la pioggia; Egli trae fuori il vento da' suoi tesori.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 [Egli è quel] che percosse i primogeniti di Egitto, Così degli uomini, come degli animali.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Che mandò segni e prodigi, in mezzo di te, o Egitto; Sopra Faraone, e sopra tutti i suoi servitori.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Che percosse nazioni grandi, Ed uccise re potenti;
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sihon, re degli Amorrei, E Og, re di Basan, E i re di tutti i regni di Canaan;
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 E diede i lor paesi per eredità, Per eredità ad Israele, suo popolo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 O Signore, il tuo Nome [è] in eterno; O Signore, la memoria di te [è] per ogni età.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Quando il Signore avrà fatti i suoi giudicii sopra il suo popolo, Egli si pentirà per amor de' suoi servitori.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Gl'idoli delle genti[sono] argento ed oro, Opera di mani d'uomini;
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Hanno bocca, e non parlano; Hanno occhi, e non veggono;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Hanno orecchi, e non odono; [Ed] anche non hanno fiato alcuno nella lor bocca.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Simili ad essi sieno quelli che li fanno; Chiunque in essi si confida.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Casa d'Israele, benedite il Signore; Casa d'Aaronne, benedite il Signore.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Casa di Levi, benedite il Signore; [Voi] che temete il Signore, beneditelo.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Benedetto [sia] da Sion il Signore, Che abita in Gerusalemme. Alleluia.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salmi 135 >