< Salmi 132 >

1 Cantico di Maalot RICORDATI, Signore, di Davide, E di tutte le sue afflizioni.
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 Come egli giurò al Signore, [E] fece voto al Possente di Giacobbe, [dicendo: ]
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 Se io entro nel tabernacolo della mia casa, Se salgo sopra la lettiera del mio letto;
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 Se do alcun sonno agli occhi miei, [O] alcun sonnecchiare alle mie palpebre;
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 Infino a tanto che io abbia trovato un luogo al Signore, Degli abitacoli al Possente di Giacobbe.
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 Ecco, noi abbiamo udito [che l'Arca era stata] nella [contrada] Efratea; [Poi] la trovammo ne' campi di Iaar.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Entriamo negli abitacoli del Signore; Adoriamo allo scannello de' suoi piedi.
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Levati, Signore; Tu, e l'Arca della tua forza, [per entrar] nel tuo riposo.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 I tuoi sacerdoti sieno rivestiti di giustizia, E giubilino i tuoi santi.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Per amor di Davide, tuo servitore, Non negare al tuo unto la sua richiesta.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Il Signore giurò verità a Davide, E non [la] rivocherà, [dicendo]: Io metterò sopra il tuo trono del frutto del tuo ventre.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Se i tuoi figliuoli osservano il mio patto, E la mia testimonianza, che io insegnerò loro; [Essi], e i lor figliuoli in perpetuo, Sederanno sopra il tuo trono.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Perciocchè il Signore ha eletta Sion; Egli l'ha gradita per sua stanza, dicendo:
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 Questo [è] il mio riposo in perpetuo, Qui abiterò; perciocchè [questo è il luogo che] io ho desiderato.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 Io benedirò largamente la sua vittuaglia; Io sazierò di pane i suoi poveri.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 E vestirò i suoi sacerdoti [di vesti] di liberazione; E i suoi santi giubileranno in gran letizia.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Quivi farò germogliare un corno a Davide; E terrò accesa una lampana al mio unto.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 Io vestirò i suoi nemici di vergogna; E la sua benda reale fiorirà sopra lui.
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Salmi 132 >