< Salmi 120 >

1 Cantico di Maalot IO ho gridato al Signore, quando sono stato in distretta, Ed egli mi ha risposto.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 O Signore, riscuoti l'anima mia dalle labbra bugiarde, E dalla lingua frodolente.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Che ti darà, e che ti aggiungerà La lingua frodolente?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 [Ella è simile a] saette acute, [tratte] da un uomo prode; Ovvero anche a brace di ginepro.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ahimè! che soggiorno in Mesec, [E] dimoro presso alle tende di Chedar!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 La mia persona è [omai] assai dimorata Con quelli che odiano la pace.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Io [sono uomo di] pace; ma, quando [ne] parlo, Essi [gridano] alla guerra.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Salmi 120 >