< Proverbi 8 >

1 LA Sapienza non grida ella? E la Prudenza non dà ella fuori la sua voce?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 Ella sta in piè in capo de' luoghi elevati, in su la via, Ne' crocicchi.
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 Ella grida presso alle porte, alla bocca della città, All'entrata degli usci [delle case],
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 [Dicendo]: Io grido a voi, o uomini principali; E la mia voce [s'indirizza] ancora al volgo.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Semplici, intendete [che cosa sia] avvedimento; E [voi] stolti, intendete [che cosa sia] buon senno.
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Ascoltate; perciocchè io proporrò cose eccellenti; L'aprir delle mie labbra [sarà] di cose diritte.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Conciossiachè il mio palato ragionerà di verità; Ma l'empietà [è] ciò che le mie labbra abbominano.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Tutti i detti della mia bocca [son] con giustizia; In essi non [vi è] nulla di torto o di perverso.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Essi tutti [son] diritti agl'intendenti, E bene addirizzati a coloro che hanno trovata la scienza.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Ricevete il mio ammaestramento, e non dell'argento; E scienza, anzi che oro eletto.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Perciocchè la sapienza [è] migliore che le perle; E tutte le cose le più care non l'agguagliano.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 Io, la Sapienza, abito nell'avvedimento, E trovo la conoscenza de' buoni avvisi.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Il timor del Signore [è] odiare il male; Io odio la superbia, e l'alterezza, e la via della malvagità, E la bocca perversa.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 A me [appartiene] il consiglio e la buona ragione; Io [son] la prudenza; a me [appartiene] la forza.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Per me regnano i re, Ed i rettori fanno statuti di giustizia.
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Per me signoreggiano i signori, Ed i principi, [e] tutti i giudici della terra.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Io amo quelli che mi amano; E quelli che mi cercano mi troveranno.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Ricchezze e gloria [son] meco; Beni permanenti e giustizia.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Il mio frutto [è] migliore che oro, anzi che oro finissimo; E la mia rendita [migliore] che argento eletto.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Io cammino per la via della giustizia, In mezzo de' sentieri della dirittura;
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 Per fare eredare il [vero] essere a quelli che mi amano, Ed empiere i lor tesori.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 IL Signore mi possedeva al principio della sua via, Avanti le sue opere, ab eterno.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Io sono stata costituita in principato ab eterno, Dal principio, avanti che la terra fosse.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Avanti che [fossero] abissi, Nè fonti, nè gorghi d'acque, io fui prodotta.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Io fui prodotta innanzi che i monti fossero profondati, Avanti i colli;
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 Mentre egli non avea [ancora] fatta la terra, nè le campagne, Nè la sommità del terreno del mondo.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Quando egli ordinava i cieli, io v'[era]; Quando egli disegnava il giro sopra la superficie dell'abisso;
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 Quando egli fermava il cielo disopra; Quando egli fortificava le fonti dell'abisso;
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 Quando egli poneva il suo termine al mare, Talchè le acque non possono trapassare il suo comandamento; Quando egli poneva i fondamenti della terra;
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 Ed era appo lui[come] un allievo, Ed era le [sue] delizie tuttodì; Io mi sollazzava in ogni tempo nel suo cospetto.
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 Io mi sollazzo nella parte abitata della sua terra; Ed i miei diletti [sono] co' figliuoli degli uomini.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 Ora dunque, figliuoli, ascoltatemi: Beati [coloro che] osservano le mie vie.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Ascoltate l'ammaestramento, e diventate savi, E non [lo] schifate.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Beato l'uomo che mi ascolta, Per vegliar tuttodì presso a' miei usci; Per istare a guardia agli stipiti delle mie porte.
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Perciocchè chi mi trova trova la vita, Ed ottiene benevolenza dal Signore.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Ma chi pecca contro a me fa ingiuria all'anima sua; Tutti quelli che mi odiano amano la morte.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.

< Proverbi 8 >