< Colossesi 3 >

1 SE dunque voi siete risuscitati con Cristo, cercate le cose di sopra, dove Cristo è a sedere alla destra di Dio.
Ikiwa tena Mungu amewafufua pamoja na Kristo, yatafuteni mambo ya juu ambako Kristo anakaa mkono wa kuume wa Mungu.
2 Pensate alle cose di sopra, non a quelle [che son] sopra la terra.
Fikirini kuhusu mambo ya juu, sio kuhusu mambo ya duniani.
3 Perciocchè voi siete morti, e la vita vostra è nascosta con Cristo in Dio.
Kwa kuwa mmekufa, na maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 Quando Cristo, [che è] la vita vostra, apparirà, allora ancor voi apparirete con lui in gloria.
Wakati Kristo atakapoonekana, ambaye ni maisha yenu, ndipo nanyi pia mtaonekana naye katika utukufu.
5 Mortificate adunque le vostre membra che [son] sopra la terra; fornicazione, immondizia, lussuria nefanda, mala concupiscenza, ed avarizia, che è idolatria.
Kwa hiyo yafisheni mambo yaliyo katika nchi yaani, zinaa, uchafu, shauku mbaya, nia mbaya, na tamaa, ambayo ni ibada ya sanamu.
6 Per le quali cose viene l'ira di Dio sopra i figliuoli della disubbidienza.
Ni kwa ajili ya mambo haya ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wasio tii.
7 Nelle quali già camminaste ancor voi, quando vivevate in esse.
Ni kwa ajili ya mambo haya ninyi pia mlitembea kwayo mlipoishi kati yao.
8 Ma ora deponete ancora voi tutte queste cose: ira, cruccio, malizia, [e] fuor della vostra bocca maldicenza, e parlar disonesto.
Lakini sasa ni lazima myaondoe mambo haya yote. Yaani, ghadhabu, hasira, nia mbaya, matusi, na maneno machafu yatokayo vinywani mwenu.
9 Non mentite gli uni agli altri, avendo spogliato l'uomo vecchio co' suoi atti;
Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
10 e vestito il nuovo, che si rinnova a conoscenza, secondo l'immagine di colui che l'ha creato.
Mmevaa utu mpya, ambao unafanywa upya katika maarifa kutokana mfano wa yule aliye muumba.
11 Dove non vi è Greco e Giudeo, circoncisione e incirconcisione, Barbaro e Scita, servo e franco; ma Cristo [è] ogni cosa, ed in tutti.
Katika maarifa haya, hakuna Myunani na Myahudi, kutahiriwa na kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa, lakini badala yake Kristo ni mambo yote katika yote.
12 Vestitevi adunque, come eletti di Dio, santi, e diletti, di viscere di misericordia, di benignità, d'umiltà, di mansuetudine, di pazienza;
Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 comportandovi gli uni gli altri, e perdonandovi, se alcuno ha qualche querela contro ad un altro; come Cristo ancora vi ha perdonati, [fate] voi altresì il simigliante.
Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ilele ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
14 E per tutte queste cose, [vestitevi] di carità, che è il legame della perfezione.
Zaidi ya mambo haya yote, muwe na upendo, ambao ndio kigezo cha ukamilifu.
15 Ed abbia la presidenza ne' cuori vostri la pace di Dio, alla quale ancora siete stati chiamati in un corpo; e siate riconoscenti.
Amani ya Kristo na iwaongoze mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii kwamba mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
16 La parola di Cristo abiti in voi doviziosamente, in ogni sapienza; ammaestrandovi, ed ammonendovi gli uni gli altri, con salmi, ed inni, e canzoni spirituali; cantando con grazia del cuor vostro al Signore.
Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa utajiri. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi, nyimbo, na nyimbo za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyo yenu kwa Mungu.
17 E qualunque cosa facciate, in parola, o in opera, [fate] ogni cosa nel nome del Signore Gesù, rendendo grazie a Dio, e Padre, per lui.
Na chochote mfanyacho, katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
18 MOGLI, siate soggette a' mariti, come si conviene nel Signore.
Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
19 Mariti, amate le mogli, e non v'inasprite contro a loro.
Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
20 Figliuoli, ubbidite a' padri e madri, in ogni cosa; poichè questo è accettevole al Signore.
Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
21 Padri, non provocate ad ira i vostri figliuoli, acciocchè non vengan meno dell'animo.
Akina baba msiwachokoze watoto wenu, ili kwamba wasije wakakata tamaa.
22 Servi, ubbidite in ogni cosa a [quelli che son vostri] signori secondo la carne; non servendo all'occhio, come per piacere agli uomini; ma in semplicità di cuore, temendo Iddio.
Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama watu wa kufurahisha tu, bali kwa moyo wa kweli. Mwogopeni Mungu.
23 E qualunque cosa facciate, operate d'animo, [facendolo] come al Signore, e non agli uomini;
Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
24 sapendo che dal Signore riceverete la retribuzione dell'eredità; poichè voi servite a Cristo, il Signore.
Mnajua ya kwamba mtapokea tuzo ya umilkaji kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
25 Ma chi fa torto riceverà [la retribuzione del] torto ch'egli avrà fatto, e non vi è riguardo a qualità di persona.
Kwa sababu yeyote atendaye yasiyo haki atapokea hukumu kwa matendo yasiyo haki aliyoyafanya, na hakuna upendeleo.

< Colossesi 3 >