< 1 Cronache 24 >

1 OR quant'è a' figliuoli d'Aaronne, i loro spartimenti [furono questi]: I figliuoli d'Aaronne [furono] Nadab, ed Abihu, Eleazaro, ed Itamar.
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Ed essendo Nadab ed Abihu morti senza figliuoli davanti al padre loro, Eleazaro ed Itamar esercitaroro il sacerdozio.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 Or Davide li distribuì secondo gli ordini loro nel lor ministerio, [essendo] Sadoc de' figliuoli di Eleazaro, ed Ahimelec de' figliuoli d'Itamar.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Ed i figliuoli di Eleazaro si trovarono in più gran numero di capi d'uomini, che i figliuoli di Itamar, quando gli spartimenti furono fatti. De' figliuoli di Eleazaro [vi erano] sedici capi di famiglie paterne, e de' figliuoli d'Itamar otto.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 E gli spartimenti furono fatti a sorte, gli uni per mezzo gli altri; perciocchè anche i capi del santuario, e [della Casa] di Dio, erano de' figliuoli di Eleazaro, e de' figliuoli d'Itamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 E Semaia, figliuolo di Natanael, Scriba, [della tribù] di Levi, li descrisse davanti al re, e davanti a' capi [del popolo], ed al sacerdote Sadoc, e ad Ahimelec, figliuolo di Ebiatar, ed a' capi delle [famiglie] paterne de' sacerdoti, e de' Leviti; una casa paterna si prendeva [de' discendenti] di Eleazaro, ed un'[altra congiuntamente di que]'d'Itamar.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 La prima sorte adunque scadde a Ioiarib, la seconda a Iedaia,
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 la terza ad Harim, la quarta a Seorim,
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 la quinta a Malchia,
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 la sesta a Miamin, la settima a Cos, l'ottava ad Abia,
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 la nona a Iesua, la decima a Secania,
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 l'undecima ad Eliasib, la duodecima a Iachim,
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 la tredicesima ad Huppa, la quartadecima a Iesebeab,
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 la quintadecima a Bilga, la sestadecima ad Immer,
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 la diciassettesima ad Hezir, la diciottesima a Pisses,
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 la diciannovesima a Petahia, la ventesima ad Ezechiele,
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 la ventunesima a Iachin, la ventiduesima a Gamul,
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 la ventesimaterza a Delaia, la ventiquattresima a Maazia.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Questi [furono] i loro ordini nel lor ministerio, [secondo i quali aveano] da venir nella Casa del Signore, secondo che era loro ordinato, sotto la condotta di Aaronne, lor padre; come il Signore Iddio d'Israele gli avea comandato.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 E QUANT'è al rimanente de' figliuoli di Levi, de' figliuoli di Amram, [vi fu] Subael; e de' figliuoli di Subael, Iedeia.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 Quant'è a' figliuoli di Rehabia, Isia [fu] il capo.
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 Degl'Ishariti, Selomot; de' figliuoli di Selomot, Iahat.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 [De' figliuoli di Hebron, Ieria era il primo], Amaria il secondo, Iahaziel il terzo, Iecamam il quarto.
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 De' figliuoli di Uzziel [fu capo] Mica; de' figliuoli di Mica, Samir.
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 Il fratello di Mica [fu] Isia; de' figliuoli d'Isia, Zaccaria [fu il capo].
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 I figliuoli di Merari[furono] Mehali, e Musi; e de' figliuoli di Iaazia, Beno [fu il capo].
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 I figliuoli di Merari, per Iaazia, [furono] Beno, e Soham, e Zaccur, ed Ibri.
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 Di Mahali [il capo fu] Eleazaro, il quale non ebbe figliuoli.
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 Quant'è a Chis, [il capo de]'suoi figliuoli [fu] Ierameel.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 E de' figliuoli di Musi [furono i capi] Mahali, ed Eder, e Ierimot. Questi [furono] i figliuoli de' Leviti, secondo le lor case paterne.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 E tirarono anch'essi le sorti, al pari de' figliuoli d'Aaronne, lor fratelli, in presenza del re Davide, e di Sadoc, e d'Ahimelec, e de' capi delle [famiglie] paterne de' sacerdoti, e de' Leviti; le principali delle [case] paterne [essendo] pareggiate ad [altre più] piccole de' lor fratelli.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.

< 1 Cronache 24 >