< לוּקָס 4 >

ישוע חזר מן הירדן מלא רוח הקודש, והרוח הובילה אותו אל המדבר – 1
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
שם ניסה אותו השטן במשך ארבעים יום. במשך כל אותו זמן לא אכל ישוע דבר, ובתום ימי הניסיון היה רעב מאוד. 2
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
”אם אתה באמת בן־אלוהים, “אמר לו השטן,”צווה על האבן הזאת להפוך ללחם!“ 3
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
אולם ישוע השיב:”כתוב:’לא על הלחם לבדו יחיה האדם, (כי על כל מוצא פי ה)‘. “ 4
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
לאחר מכן העלה השטן את ישוע, בחזיון רגעי הראה לו את כל המדינות המפוארות שבעולם ואמר: 5
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
”אני אתן לך את כל הממלכות המפוארות האלה ואת כבודן – כי לי נמסר השלטון ורשאי אני לתת אותו למי שארצה – אבל בתנאי אחד: עליך לכרוע ברך ולהשתחוות לפני.“ 6
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
אולם ישוע השיב לו:”אך כתוב:’לה׳ אלוהיך תשתחווה, ואותו לבדו תעבוד‘. “ 8
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
השטן לקח את ישוע לירושלים, העלהו על גג בית־המקדש ואמר:”אם אתה באמת בן־אלוהים, קפוץ למטה! 9
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
הרי כתוב בתנ״ך:’כי מלאכיו יצווה לך לשמרך… 10
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
על כפיים ישאונך פן תיגוף באבן רגלך‘. “ 11
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
”אולם כתוב:’לא תנסה את ה׳ אלוהיך‘, “השיב לו ישוע. 12
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
כאשר סיים השטן לנסות את ישוע עזב אותו לנפשו עד לעת מועד. 13
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
לאחר מכן חזר ישוע לגליל כשהוא מלא בכוח רוח הקודש, ועד מהרה התפרסם בכל האזור. 14
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
ישוע לימד את העם בבתי־הכנסת וכולם הללו ושיבחו אותו. 15
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
ישוע בא אל נצרת – העיר שבה בילה את ילדותו – ובשבת הלך כמנהגו לבית־הכנסת. כשקם על רגליו כדי לקרוא את ההפטרה, 16
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
הגישו לו את ספר ישעיהו. ישוע פתח את המגילה וקרא בקול: 17
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
”רוח ה׳ עלי, יען משח ה׳ אותי לבשר ענוים; שלחני לחבש לנשברי לב, לקרוא לשבוים דרור ולאסורים – פְּקַח־קוֹחַ; 18
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
לקרוא שנת רצון לה׳.“ 19
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
ישוע גלל את המגילה, החזירה לחזן וישב במקומו. כל באי בית־הכנסת נעצו בו את עיניהם בציפייה, 20
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
וישוע הוסיף:”היום התקיימו דברי הפסוקים האלה בקרבכם!“ 21
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
כולם הקשיבו לדבריו והתפלאו על דברי החן והחוכמה שיצאו מפיו.”איך ייתכן הדבר?“שאלו איש את רעהו.”האין זה בנו של יוסף?“ 22
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
ישוע ענה להם:”ודאי תאמרו לי:’רופא, רפא תחילה את עצמך!‘או במילים אחרות:’מדוע אינך מחולל כאן, בעיר מולדתך, את הניסים והנפלאות שחוללת בכפר־נחום?‘ 23
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
אני אומר לכם: אין נביא בעירו! את הנביא מכבדים בכל מקום חוץ מאשר בביתו ובין בני־עמו. 24
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
”בימי אליהו הנביא לא ירד גשם במשך שלוש וחצי שנים, והבצורת גרמה לרעב גדול בכל הארץ. למרות שהיו בישראל אלמנות רבות שרעבו ללחם, 25
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
לא שלח אלוהים את אליהו אל אף אחת מהן! אלוהים שלח את אליהו רק אל אלמנה לא יהודיה בעיירה צרפת שבצידון. 26
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
או קחו לדוגמה את אלישע; אף כי בימי אלישע הנביא היו מצורעים רבים בישראל, הוא לא ריפא איש מהם, אלא דווקא את נעמן הארמי.“ 27
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
דברי ישוע עוררו את זעמם. 28
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
הם קפצו מכיסאותיהם ודחפו אותו אל מחוץ לעיר, אל פסגת ההר שעליו נבנתה נצרת, במטרה להשליכו במדרון. 29
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
אולם ישוע התחמק מהם והלך לדרכו. 30
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
לאחר מכן הלך ישוע לכפר־נחום שבגליל, ומדי שבת לימד בבית־הכנסת. 31
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
גם כאן נדהמו השומעים, כי ישוע דיבר בסמכות בלתי רגילה. 32
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
פעם כשלימד ישוע בבית־הכנסת צעק לפתע איש אחד אחוז רוח שד טמא: 33
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
”מדוע אתה מטריד אותנו, ישוע מנצרת, האם באת להשמיד את השדים? אני מכיר אותך; אתה בנו הקדוש של אלוהים!“ 34
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
ישוע נזף בשד וציווה עליו:”שתוק וצא החוצה!“השד השליך את האיש על הרצפה לעיני כולם, ויצא ממנו בלי לפגוע בו שוב. 35
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
כולם נדהמו ושאלו איש את רעהו במבוכה:”מה המיוחד בדברי האיש הזה עד כי אפילו שדים מצייתים לו?“ 36
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
עד מהרה התפרסם סיפור המעשה בכל האזור. 37
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
לאחר שעזב ישוע את בית־הכנסת, הלך לביתו של שמעון וראה את חמותו של שמעון קודחת מחום.”אנא, רפא אותה“, התחננו לפניו כולם. 38
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
ישוע עמד ליד מיטתה וגער בקדחת. מיד ירד החום, והיא קמה ממיטתה והכינה להם אוכל. 39
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
עם שקיעת השמש הביאו תושבי הסביבה אל ישוע חברים ובני משפחה שחלו במחלות שונות. ישוע הניח את ידיו עליהם וריפא אותם. 40
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
ישוע גם גירש שדים מאנשים רבים, ובצאתם נהגו השדים לקרוא בקול:”אתה הוא בן־האלוהים!“אולם ישוע השתיק אותם, בגלל שהם ידעו שהוא המשיח. 41
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
למחרת, השכם בבוקר, הלך ישוע למקום שומם כדי להתבודד. המוני העם חיפשו אותו בכל מקום, וכשמצאו אותו התחננו לפניו:”אנא, אל תעזוב אותנו; הישאר איתנו בכפר־נחום.“ 42
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
אולם ישוע השיב להם:”עלי לבשר את דבר מלכות האלוהים גם בערים אחרות, כי זוהי מטרת שליחותי.“ 43
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
וישוע המשיך ללמד בבתי־הכנסת השונים שבאזור יהודה. 44
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< לוּקָס 4 >